MWENYEKITI WA CCM SINGIDA, AISHAMBULIA CHADEMA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

MWENYEKITI WA CCM SINGIDA, AISHAMBULIA CHADEMA


Mwenyekiti wa CCM Singida vijijini, Narumba Hanje akisoma Agano jipya kitabu cha Wagalatia mbele ya mkutano mkuu wa UVCCM Singida vijijini juzi.
Kushoto ni katibu wa UVCCM Singida vijijini Rubein na anayefuata ni mwenyekiti wa jumui ya ya wazazi Singida vijijini, Elia Digha.
Baadhi ya wajumbe wa mkutano mkuu wa UVCCM Singida vijijini.Picha zote na Nathaniel Limu
---
Na Nathaniel Limu-Singida.
Mwenyekiti wa CCM Singida vijijini Narumba Hanje, amekitabiria Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kwamba hakitaingia Ikulu milele kwa madai kuwa kimepoteza mwelekeo baada ya  kuanza kutumia mbinu chafu ambazo hazitawasaidia kufikia lengo lao.
Hanje ametoa utabiri huo wakati akifungua mkutano mkuu wa Jumuiya ya umoja wa vijana (UVCCM) uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa shirika la Pride Singida Mjini.
Alisema CHADEMA sasa kimeacha kuwaeleza wananchi kitawafanyia nini ili waweze kuleta maendeleo endelevu,  na badala yaje  kueneza fitina, hasira, uadui, uzushi.

Aidha, Hanje amedai kuwa Chama hicho kimeundwa, ‘kiundugunaizesheni’ na kwamba hakina demokrasi na kuwa na mwonekano wa taasisi binafsi, na kuongeza kuwa kimepoteza muda mwingi  kwa kuzunguka na kufanya maandamano ambayo hayana tija kwa wananchi.
Mwenyekiti huyo amedai chama hicho kimeonyesha dhahiri kwamba hakiwatakii mema Watanzania baada ya kuanza kuwadanganya na kuwashawishi  wasichangie  maendeleo  kwa madai kwamba jukumu la kuleta maendeleo ni la serikali pekee.

“Sisi hapa mjini, tunachangia mambo mengi hata ya uzoaji wa takataka, sembuse maendeleo”, alihoji na kuongeza “CHADEMA hawana ubavu tena wa kuchukua nchi, wamepoteza mwelekeo, wamefikia mahali wanaifananisha Tanznaia na Misri”.

Hanje alisema CHADEMA ni ya kuogopwa kama ukoma, kwa madai kwamba viongozi wa  chama hicho,wanatumia nafasi zao kujaza watu wa ukoo wao  katika nafasi mbali mbali za uongozi.
Katika kuujengea nguvu utabiri wake huo, mwenyekiti  huyo alisoma Agano jipya kitabu cha Wagalatia 5 mstari mdogo kuanzia 19-21.

Pamoja na mambo mengine, mistari hyo inasema ‘Fitina, wivu, hasira, husuda na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo, nawaambia kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo, hawataurithi ufalme wa Mungu.’

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages