Saturday, June 02, 2012

DONT MISS THIS ONE... Leggings VS Single Button @club much more

DONT MISS THIS ONE... Leggings VS Single Button @club much more ON this Friday 8th June 2012..... vip.. Better to be in the dresscode

RAIS KIKWETE AKUTANA NA RAIS WA SOMALIA ARUSHA LEO

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais Sheikh Shariff Ahmed aliyekutana naye leo june 2, 2012 jijini Arusha. Pamoja na mambo mengine Rais Kikwete na mgeni wake waliongelea hali ya usalama katika nchi hiyo ya pembe ya  Afrika na pia akamhakikishia Rais huyo ushirikiano wa kila aina katika kuhakikisha utulivu unarejea nchini Somalia. PICHA NA IKULU

LIGHTNESS MICHAEL NDIYE REDDS MISS DODOMA 2012

Mshindi Wa Taji la Redds Miss Dodoma 2011 akisubiri Kumvalisha Taji Mshindi ambaye atatangazwa katika shindano la Kuwania Taji la Redds Miss Dodoma 2012
Mshindi wa Taji la Redds Miss Dodoma 2012 (katikakati) Lightness Michael akiwa katika picha ya Pamoja na Mshindi wa Pili (Kulia)  Berinda Mdogo na Mshindi wa Tatu wa taji la Redds Miss Dodoma 2012 (Kushoto) Nulsa Magambo Mara baada ya Mshindi wa Taji la Redds Miss Dodoma Kumalizika hapo Jana
Washiriki wa Kinyanganyiro Cha Kuwania Taji la Redds Miss Dodoma Wakiwa Katika Picha ya Pamoja kabla ya Kutangazwa Washiriki walioingia Tano Bora
 Muda wa Maswali Ukawadia Kwa washiriki walioingia katika tano bora
 Baadhi ya washiriki walipokua wakipita Jukwaani kwa Mara ya kwanza
 Muda wa Kuonyesha Vipaji sasa hapo ni mauno kwa kwenda mbele
 Vazi la Ufukweni hilo
 Washiriki walioingia hatua ya tano bora
 Jaji mkuu akisoma majin ya washiriki walioingia tano bora
Muda wa kipaji na Mshiriki huyu akaja na kipaji cha kuimba kihindi na kucheza kuch kuch
 Majaji wakiwa makini katika kuhakikisha wanatoa mshiriki anayefaa na mwenye vigezo vyote vinayohitajika
Msanii wa Bongo Fleva Dully Sykes akitoa Burudani kwa washabiki waliohudhuria katika shindano la kuwania taji la Redds Miss Dodoma 2012 lililofanyika jana katika ukumbi wa kilimani
 Baadhi ya Wadau waliojitokeza kushuhudia Kinyanganyiro Hiko huku wengine wakisakata rumba mara baada ya Dully Sykes Kuwakuna Vilivyo
Waratibu wa Shindano hilo wakiwa katika Picha ya Pamoja
 Hawa ndio waliokunwa vizuri na Show ya Msanii wa Bongo Fleva Dully Sykes
Mmiliki wa mtandao wa Lukaza blog (Wa Kwanza Kushoto) Josephat Lukaza Akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa UDOM waliojitokeza kuwashangilia Wanafunzi wenzao walioshiriki shindano hilo
Mshindi wa Kwanza wa Taji la Redds Miss Dodoma 2012 Lightness Michael akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa Shindano hilo.

Rais Kikwete akutana na Mmiliki wa klabu ya Portsmouth Dkt. Sulaiman Al Fahim Ikulu jijini Dar es Salaam leo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Royal Group ya Saudi Arabia, Dkt. Sulaiman Al Fahim wakati walipokutana leo, Jumamosi, Juni 2, 2012, Ikulu Dar es Salaam. Dkt. Al Fahim ambaye ni mwenyekiti wa zamani na mmiliki mwenza wa Klabu ya soka ya Portsmouth ya Uingereza yuko nchini kuangalia uwezekano wa kuwekeza katika uchumi wa Tanzania. Dkt. Al Fahim pia ndiye aliyeongoza mazungumzo na kununuliwa kwa klabu bingwa ya Ligi Kuu ya Uingereza ya Manchester City na Kampuni ya Arabuni.
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mzungumzo na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Royal Group ya Saudi Arabia, Dkt. Sulaiman Al Fahim
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Royal Group ya Saudi Arabia, Dkt. Sulaiman Al Fahim mara baada ya  mazungumzo yao Ikulu leo. (Picha na fredy Maro).

ROLI LANUSULIKA KUUNGUA MOTO KIMARA MWISHO JIJINI DAR ES SALAAM

Gari aina SCANIA lenye namba za usajili T 587 ABV lilokuwa limebeba mafuta ya Petroli limeponea chupuchupu kulipuka baada ya tairi la mbele kuwaka moto baada ya wasamaria wema kuwahi kuzima moto uliokuwa ukiwaka kama lilivyokutwa na kamera yetu maaeneo ya Kimara mwisho jijini Dar es salaam leo. (PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE)

TEMBELEA MTANDAO MPYA WA THIS DAY MAGAZINE

Karibuni wadau wote katika Magazine mpya ambayo inapatikana katika mtandao pekee,lengo kubwa la Magazine hii ni kuwapasha, si Habari pekeyake lakini pia pamoja na mambo mengine mengi ambayo ukifungua mtandao utayaona. kama ungependa kutuma habari kulingana na Categories utakazo ziona  tunawakaribisha sana.Pia wataarifu ndugu,jamaa na marafiki. Tunatanguliza Shukurani.
Link: http://thisdaymag.blogspot.com/
Kwa mawasiliano: thisdaymagazine@live.com

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA KATIKA MKUTANO WA SADC LUANDA ANGOLA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe (kulia)  wakizungumza na Rais wa Zambia, Michael Santa katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi  Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC uliofanyika Juni 1, 2012, Luanda Angola. Mheshimiwa Pinda alimwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika Mkutano huo.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akifurahia katika mazungumzo kati yake na Waziri Mkuu wa Kwanza wa Namibia, Hage Geigob wakati walipokutana  katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC, Luanda , Angola Juni 1, 2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MWENGE WA UHURU WAKIMBIZWA WILAYA YA NAMTUMBO

Mwenge wa Uhuru ukikimbizwa kuingia katika wilaya ya Namtumbo kuanza kazi ya kuhamasisha shughuli za maendeleo ukitokea wilaya ya Songea.Jumla ya miradi  11 yenye thamani zaidi ya shilingi milioni 400 imezinduliwa,imewekewa mawe ya msingi na kufunguliwa.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kapteni Honest Mwanossa akichanganya mbolea wakati wa uzinduzi wa shamba la michungwa  kwa kutumia  mbolea vunde kwa kuongeza ubora wa mazao na hifadhi ya mazingira katika kijiji cha Msindo wilaya ya Namtumbo.Shamba hilo lenye ukubwa wa hekari mbili na nusu linamilikiwa na Mzee Venant Haule (mwenye fulana nyekundu).
Mtoto Mezea Seif wa darasa la kwanza katika shule ya msingi Njalamatata akiwa ameshika Mwenge wa Uhuru  wakati ulipokuwa katika kijiji hicho wilaya ya Namtumbo kwa kazi ya kuhimiza shughuli za maendeleo  jana.
-Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kapteni Honest Mwanossa akizindua mradi wa kisima cha maji safi ya kunywa kwa ajili ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya Utwango wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.Kulia ni Mbunge wa jimbo la Namtumbo Vita Kawawa.
 Raia wa Marekani aliyefahamika kwa jina moja la Penzia akiwa ameshika Mwenge wa Uhuru wakati uliposimama katika kijiji cha Hanga kutoa ujumbe kwa wananchi kuhusu umuhimu wa wananchi kujiandaa kuhesabiwa ifikiapo Agosti 26,2012.

Na Revocatus A.Kassimba
Afisa Habari
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Ruvuma

WINFRIDA PAULO AIBUKA MSHINDI WA MISS REDDS 2012 MKOANI MBEYA

 HAPA AKIVISHWA  ILE KOFIA YA USHINDI
 AKIWA NA FURAHA MUDA MFUPI BAADA YA KUVISHWA TAJI LA USHINDI
KUTOKA KUSHOTO NI MSHINDI WA PILI ANAITWA SABRINA ABDUL NA KULIA NI MSHINDI WA TATU ANAITWA CAREEN ELIAS .Picha na Mbeya Yetu Blog

Friday, June 01, 2012

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Join me on Facebook Follow me on Twitter Find me on Youtube