Featured Posts

Wednesday, May 22, 2013

BREAKING NEWS: MATUKIO YANAYOENDELEA MTWARA MUDA HUU BAADA YA MABOMU KURINDIMA

Mabomu yanapigwa mfululizo maeneo ya Magomeni-Mtwara . Takriban mabomu 20 na ushee mpaka sasa. Na wanaendelea kupiga mabomu. Sasa hali si shwari kila eneo, wakionekana watu watatu wanaongea maongezi maaskari wanapiga mabomu. Mabavu yamechukua mkondo wake. Wananchi wamejifungia majumbani mwao. Chuki dhidi ya Polisi yaimarika. Polisi wanapiga mabomu bila mwelekeo. Magomeni na sokoni kimenuka, mabomu yanarushwa na wananchi wanakimbia ovyo. 
Kituo kimoja cha habari kinachorusha habari za bunge chazuia mawimbi yake kwa Mkoa wa Mtwara hivyo hakisikiki(Redio na TV). Na kimewanyima haki wananchi wa Mtwara ya kupata taarifa.(Hatimaye wamerejesha matangazo yao) 
Waziri wa Nishati amesoma hotuba yake kwa hisia kali na mbwembwe. Mwishoni amesema bomba la gesi linajengwa kutoka Mtwara kwenda Dar.  Maduka yote yamefungwa, baa zimefungwa, hakuna huduma za usafiri, ofisi za serikali zimepwaya kimsingi hakuna lolote linalofanyika Boda boda zinazoonekana maeneo ya Nkanaledi na abiria zinapigwa mawe. 
Makachero nao wanajifanya madereva wa boda boda na Bajaji, Tax wengine wanatembea na magari ya Serikali.  Maeneo yote yametawaliwa na ukimya.
Credit: Zeddlicious Blog

VICHWA VYA HABARI VILIVYOPAMBA KWENYE MAGAZETI YA LEO JUMATANO




 
 

JESHI LA POLISI MKOANI DODOMA LINAWASHIKILIA WATU WANNE BAADA YA KUWAKAMATA WAKITENGENEZA POMBE HARAMU

 Kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma David Misime akiwaonyesha wandishi wa Habari Mabomba ya plastik Inayotumika kama Mitambo ya kutengenezea Pombe Haramu Aina ya Gongo Mara Baada ya kuikamata wilayani Kongwa jana.
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma David Misime Akifungua Moja ya Madumu yaliyokamatwa na  Pombe Haramu ya Gongo yaliyokamatwa Wilayani Kongwa huku watu wanne wakishikiliwa na jeshi hil;o.
Haya ndio mabomba ya kutengenezea pombe haramu  PICHA NA JOHN BANDA.

Airtel yazindua ofa kabambe kupiga simu kwenda nje ya nchi



 Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Beatrice Singano (kushoto) na Meneja Biashara za Kimataifa wa Kampuni hiyo, Prisca Tembo (wa pili kutoka kulia) wakizindua huduma mpya ya kupiga simu kwenda India kwa gharama nafuu. Wengine ni Balozi wa India hapa nchini, Debnath Shaw (katikati) na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Sunil Colaso.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Sunil Colaso (wa pili kutoka kulia), akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma mpya ya kupiga simu kwenda India kwa gharama nafuu. Wengine ni Meneja Biashara za Kimataifa wa Kampuni hiyo, Prisca Tembo (kulia), Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni hiyo, Beatrice Singano na Balozi wa India hapa nchini, Debnath Shaw.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Beatrice Singano (kushoto) akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma mpya ya kupiga simu kwenda India kwa gharama nafuu. Wengine wanaofuatia ni Balozi wa India hapa nchini, Debnath Shaw, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Sunil Colaso na Meneja Biashara za Kimataifa wa Kampuni hiyo, Prisca Tembo.

ALIKUFA KWA NGOMA BY MWANA FA.NYIMBO ILIYOTAMBA MIAKA YA NYUMA

NEW IPHONE 6: KWA WAPENZI WA IPHONE HII INAKUHUSU.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MKUTANO WA 14 WA BARAZA LA USIMAMIZI WA MAWASILIANO AFRIKA, JIJINI DAR JANA

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akifungua rasmi Mkutano wa 14 wa baraza la usimamizi wa Mawasiliano Afrika, uliofunguliwa  Mei 21, 2013 kwenye Hoteli ya Double Tree jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongoza na Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Prof. John Mkoma, wakati akiondoka kwenye chumba cha mkutano baada ya kufungu rasmi mkutano huo wa 14 wa baraza la usimamizi wa Mawasiliano Afrika, uliofunguliwa Mei 21, 2013 kwenye Hoteli ya Double Tree jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo kutoka nchi za Afrika, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akifungua rasmi mkutano huo wa 14 wa baraza la usimamizi wa Mawasiliano Afrika, uliofunguliwa  Mei 21, 2013 kwenye Hoteli ya Double Tree jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu na baadhi ya washiriki wa mkutano huo, baada ya ufunguzi.

JESHI LA POLISI MKOANI IRINGA LAMSHIKILIA DIWANI WA CHADEMA KUFUATIA VURUGU ZILIZOTOKEA IRINGA JUMAPILI

dwn 863ab
Kufuatia vurugu za wamachinga Mkoani IRINGA Juzi jumapili, Polisi Mkoani humo  wamemkamata Diwani wa kata ya  Mivinjeni FRANK NYALUSI kupitia tiketi ya CHADEMA nakufanya idadi ya waliokamatwa kufuatia sakata hilo kufikia 77.PICHANI ni  Diwani FRANK akiwahutubia wananchi kwenye moja ya mikutano yake ya kichama.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AKUTANA NA MWENYEKITI MSTAAFU WA KAMATI TENDAJI YA BUNGE LA CHINA NA UJUMBE WAKE.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Makamu Mwenyekiti Mstaafu wa Bunge la China, Lu Youngxiang (wa pili kushoto) aliyeongozana na ujumbe wake wakati walipofika Ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam, jana kwa mazungumzo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti Mstaafu wa Bunge la China, Lu Youngxiang (wa tatu kushoto) aliyeongozana na ujumbe wake baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam, jana.

FANI YA UANDISHI WA HABARI IMEVAMIWA, TUSIPOZIBA UFA TUTAJENGA UKUTA

Pichani ni waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakiwa katika maandamano ya amani (Picha na Maktaba).
 ---
Watu wengi kwa sasa wameibuka na kutokea kuipenda fani ya uandishi wa habari bila kujua misingi na miiko ya uandishi wa habari. Tatizo moja ambalo limeonekana ni kubwa sana ni utandawazi ambao umekuwepo na kutokea ibuko la kila kijana kufungua gazeti tando (blog).

Hatukatai kuja kwa magazeti tando ila naomba tujiulize, yanatumika ipasavyo ama ndiyo limekuwa ni wimbi vamizi lenye kutoa ama kusambaza habari hata zile zisizokuwa na vyanzo kamili na visivyojitosheleza.Kwa sasa imezuka tabia ya wanaojiita wamiliki wa magazeti tando,wengi wao kukopi na kupaste vitu wanavyoviokota katika mitandao ya kijamii ikiwemo Twitter, facebook na mingine mingi.

Sina nia ya kumsema mtu bali napenda tuelimishane kama vijana wenzangu,ambao wametokea kuipenda fani ya uandishi wa habari, wakumbuke kuwa fani ya uandishi wa habari ina miiko na maadili yake, mfano. Katika kuandika habari za mazingira, siasa, elimu, uchumi, michezo, burudani ukiangalia habari hizi zote zina misingi na miiko yake. Leo hauwezi kumchukua mwandishi wa habari za michezo ukamwambia aandike habari za uchumi kwa vile hatakuwa na takwimu za uchumi na hata akiandika hiyo habari na kuisoma utakuwa unajiuliza maswali mengi bila kupata majibu.

Vile vile ni vizuri vijana wenzangu kutambua kuwa kila kazi ina mipaka na misingi yake, juzi juzi nilisoma habari katika gazeti tando moja wapo ikisema, 'ALIYEONGOZA MAANDAMANO YA IRINGA MHESHIMIWA MCHUNGAJI MSIGWA ASWEKWA NDANI' nilijiuliza maswali mengi ambayo kiukweli nilikosa majibu yake, kuona huyu aliyeandika hiki kichwa cha habari kweli amepitia fani ya uandishi wa habari ama ndio ule upepo vamizi?

Maana unapoandika habari za mahakamani, polisi kuna misemo yake, hauwezi kumuhukumu mtu moja kwa moja kwa kusema fulani ni mwizi, hata hao polisi ambao huwa wanakwenda kukamata watu eneo la tukio hawawezi kusema fulani ni mwizi mpaka apelekwe mahakamani ndipo sheria ichukue mkondo wake na kumbaini huyo aliyekamatwa ni mwizi.

Naomba tufike mahali tuheshimu utu wa watu na kuepuka udhalilishaji wa bila kujua naamini baadhi ya vijana wengi walioamua kufungua magazeti hayo tando ambayo yanatoa habari, hawana taaluma ya uandishi wa habari.

Napenda kuwapongeza wale walioamua kufungua magazeti tando katika milengo yao tofauti ikiwemo kutoa habari kwa njia ya 'kufundisha masuala ya urembo, mapishi, kuwasaidia kuwatangaza vijana katika muziki na hata wale walioamua kuandika habari zao binafsi.

Nayasema yote hayo kwa vile kumezuka wimbi la vijana wanaotaka kuichafua fani ya uandishi wa habari na ionekane si fani ya watu walioenda shule bali ni ya wahuni tu wasiojua mambo, naomba vijana tuelimike na tujifunze kwa watu wanayoyajua mambo ili tuweze kufika mbele zaidi.
Namalizia kwa kusema tusipoziba ufa tutajenga ukuta.

Asanteni sana kwa kusoma.
Imeandikwa na Cathbert A. Kajuna
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
 
Join me on Facebook Follow me on Twitter Watch Me On Youtube