Mbunge wa Temeke, Zuberi Mtemvu, ( kushoto) na Mbunge wa Ilala, Iddi Hassani Zungu wakisoma dua.
WANAMUZIKI 13 wa kundi la muziki wa taarabu la Five Star waliofariki katika ajali ya gari katika eneo la Hifadhi ya Taifa ya Mikumi, Morogoro, mwezi Machi mwaka huu, jana walifanyiwa hitma katika ukumbi wa PTA uliopo katika Viwanja vya Maonyesho ya Biashara vya Sabasaba jijini Dar es Salaam. Miongoni mwa mamia ya watu waliohudhuria ni pamoja na Mbunge wa Temeke, Zuberi Mtemvu, na Mbunge wa Ilala Hassani Zungu.
WANAMUZIKI 13 wa kundi la muziki wa taarabu la Five Star waliofariki katika ajali ya gari katika eneo la Hifadhi ya Taifa ya Mikumi, Morogoro, mwezi Machi mwaka huu, jana walifanyiwa hitma katika ukumbi wa PTA uliopo katika Viwanja vya Maonyesho ya Biashara vya Sabasaba jijini Dar es Salaam. Miongoni mwa mamia ya watu waliohudhuria ni pamoja na Mbunge wa Temeke, Zuberi Mtemvu, na Mbunge wa Ilala Hassani Zungu.
Baadhi ya watu wakiwasili katika hitma hiyo.
Mbunge wa Temeke, Zuberi Mtemvu (katikati) akiongea jambo na mwanamuziki Matei Joseph (kushoto) na Saidi Fela mara baada ya kuwasili.
Miongoni mwa mamia waliojitokeza katika kisomo hicho.
Mwanamuziki wa bendi ya TOT Taarab, Khadija Omar Kopa (kushoto) akiongea na meneja wa TMK Wanaume Family, Saidi Fela.
Khadija kopa (kushoto) akiwa na Mwanahawa Ally mwanamuziki aliyenusirika katika ajali hiyo.
Zuberi Mtemvu ( kushoto) na Iddi Hassani Zungu wakifuatilia kisomo hicho.
...Wakipata msosi.
Baadhi ya waalikwa wakitoka nje baada ya kisomo hicho.
PICHA ZOTE NA ISSA MNALLY / GPL
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)