KILI TAIFA CUP YAKARIBIA KUANZA, TBL YATOA MAFUNZO - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

KILI TAIFA CUP YAKARIBIA KUANZA, TBL YATOA MAFUNZO

Mkurugenzi Masoko wa Kampuni ya TBL, David Minja, akimkabidhi jezi ya Yanga, Nahodha wa timu ya waandishi wa habari mashabiki wa Yanga, Muhidin Sufiani AKA Sufianimafoto, kwa ajili ya mchezo wa kirafiki na wenzao wa Simba, baada ya mafunzo hayo ambapo katika mchezo huo Yanga ilishinda 1-0. Katikati ni Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah. Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah (kushoto) akimkabidhi jezi Nahodha wa Timu ya waandishi wa habari Mashabiki wa Simba, Amri Masale, kwa ajili ya mchezo wa kirafiki na wenzao wa Yanga.
Mkurugenzi Masoko wa Kampuni ya Bia ya TBL, David Minja, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mafunzo maalum yaliyotolewa na kampuni hiyo kwa waandishi wa habari za michezo kuhusu michuano ya Kili Taifa Cup, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya michuano hiyo. Mafunzo hayo yalifanyika leo kwenye Ukumbi wa South Beach Kigamboni Dar es Salaam.
Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe, akisisitiza jambo na kufafanua kuhusiana na mashindano hayo.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages