BOSI WA KONYAGI APASUA JIPU, alia na magazeti yanayochafua kampuni yake inayotamba kwa sasa nchini - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

BOSI WA KONYAGI APASUA JIPU, alia na magazeti yanayochafua kampuni yake inayotamba kwa sasa nchini


Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL),  David Mgwassa (kulia) akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Dar es Salaam, ambapo alilalamikia kitendo cha baadhi ya magazeti yenye uhusiano wa nchi jirani, yanayotumika kuchafua bidhaa za TDL. Kushoto ni Meneja Masoko wa TDL, Joseph Chibehe. Yafuatayo ni maelezo ya Bw. Mgwassa
Baadhi ya wanahabari wakisikiliza kwa makini wakati Mgwassa akilalamikia jambo hilo


Tumeanza kuona magazeti yenye affiliation na nchi za jirani yakitumika ku misrepresent products za TDL.


Articles ninazozungumzia zilichapishwa tarehe 2 may 2013 na tarehe 6 may 2013, kupotosha umma, na kupindisha ukweli. kwa sababu mawasiliano ya kisheria yanafanyika sitataja ni magazeti gani yanahusika, lakini nina uhakika yana uhusiano mkubwa wa kibiashara na nchi jirani.
Ushauri wangu ni kuwa magazeti ya Tanzania, yaepukane sana na vitu vinavyoonyesha kuwa kuna muelekeo wa kurepresent matakwa ya nchi tofauti na kupuuza matakwa ya kitanzania
 

Kitendo cha kujaribu kuoanisha brand ya Konyagi na accidents za magari au piki piki , ni ya upotoshaji mkubwa wa jamii ya kitanzania, kwani hakuna bia, hakuna pombe za kienyeji au pombe kali. Huu ni uhuni na ujinga mtupu
Sisi TDL hatuogopi ushindani, sio ushindani wa humu Tanzania, na nasema tutaendelea kuuza products zetu zinazozalishwa Tanzania, huko Uganda, Kenya south Sudan, Rwanda na Burundi, licha ya matatizo makubwa tunayopata.


Na tutaendelea kuwasiliana na mabalozi, wa nchi husika, EAC office na wizara zenye mamlaka katika kukuza soko la pamoja la Jumuia ya Afrika ya Mashariki, kuhusu changamoto za kibiashara tunazozipata.


Kama nilivyozungumza mwanzo sisi hatuzalishi Konyagi tuu, bali tunazalisha Zanzi cream, Knights, Viceroy brandy , siyo kwa sababu hatuwezi kuagiza, bali kwa  kutumia watanzania katika uzalishaji na kuwapa ajira. Msitufananishe sisi na watu wanaoleta makatoni ya pombe kutoka Ireland au Uingereza, sisi tuko tofauti na mahitaji ya nchi hii tunayajua.
Raisi wetu Dr Kikwete kila siku anasema issue hiyo hiyo, value added , value added, mbona masikio yenu mnafunga?


Naomba niwaeleze ukienda South Africa leo utaona kila aina ya magari mapya, utaona Toyota, utaona Nissan utaona Mercedez benz , utaona Kia na kadhalika, lakini magari yote hayo yanaundwa South Afrika, huwezi kukuta gari imetengenezewa Singapore, nia ni kuhakikisha kuwa wenyeji wanapata kazi, na approach yetu  TDL ni same.


Sioni kati ya nyie mtu ambaye anamchukua mtoto wake kumpeleka Nairobi au Dubai, kumtafutia kazi, wote mnawaleta kwetu, hata leo wengine wananiomba kazi, kwa hiyo naomba sana mtu akikujaza akili au upumbavu, na wewe jaribu kuchanganya na akili nzuri za kwako. Ahsanteni sana


No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages