TWANGA YAZINDUA (TWANGA FACEBOOK FANS CLUB PAGE YAO) MZALENDO PUB USIKU HUU - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

TWANGA YAZINDUA (TWANGA FACEBOOK FANS CLUB PAGE YAO) MZALENDO PUB USIKU HUU

 
Kiongozi na mwimbaji wa bendi ya African Stars Lwiza Mbutu akiimba katika onesho la bendi hiyo linalofanyika usiku huu kwenye klabu ya Mzalendo Makumbusho jijini Dar es salaam ambapo kampuni ya ASET inazindua mpango wake wa Twanga Facebook Fans Club unaokutanisha marafiki wa bendi hiyo katika mawasiliano ya Mtandao lengo likiwa kusherehekea pamoja na wadau wake mbalimbali wanaoisapoti bendi hiyo kupitia mitandao ya kijamii. Fullshangweblog iko ukumbini hapo ikikumuvuzishia matukio haya moja kwa moja usiku huu kutoka Mzalendo Pub Makumbusho jijini Dar es salaam.
 
Janet Isinika mmoja wa waimbaji wakongwe katika bendi hiyo akifanya vitu vyake jukwaani, siku moja aliwahi kuniambia unapokuwa mwanamuziki hata kama una matatizo unatakiwa kusahau kila kitu unapokuwa jukwaani ili kumburudisha na kumpa raha yule anayekutazama na kukuzikiliza.
Mpiga gitaa la besi katika bendi hiyo Jojo Jumanne akifanya vitu vyake huku wanenguaji wa bendi hiyo wakicheza kwa staili ya aina yake.
Mhh! hii sijajua ni staili gani lakini yote ni kushangweka tu wadau wetu.
Hapa shoo imekolea kama unavyowaona wanenguaji wa bendi ya African Stars wakifanya vitu vyao jukwaani.
Janet Isinika akienda sambamba na wanenguaji wa kiume wa bendi ya African Stars kama wanavyoonekana wakiwajibika jukwaani.Picha Kwa Hisani ya Full Shangwe Blog

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages