
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Hussein Mwinyi akisalimiana
na mmoja wa wagonjwa wa saratani waliolazwa katika wodi hospitalini
hapo. Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Dkt. Twalib Ngoma alisema hivi sasa
watanzania 100 wanafariki kwa ugonjwa wa saratani na asilimia 35 ya
ugonjwa huo unaweza kuzuilika.

Mh. Dkt. Mwinyi akipata maelezo toka kwa mtaalam(hayupo pichani) wa
mashine inayosaidia kuchanganya dawa za mionzi na kuchunguza wagonjwa
mbalimbali ( Nuclear Medicine)iliyopo katika jengo jipya la hospitali ya
Ocean Road.

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii katika chumba cha mionzi. Idadi ya
wagonjwa wa saratani imeongezeka toka wagonjwa 2,000 mwaka 2002 hadi
kufikia wagonjwa 5,000 hivi sasa.

Baadhi ya watumishi wa Taasisi ya Saratani Ocean
Road wakimsikiliza Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii kwenye ukumbi wa
Mkutano hospitalini hapo.Picha zote na Catherine Sungura-Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)