Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Yaanza kuutangaza Mradi wa Mapitio ya Mfumo wa Utoaji Haki katika Mashauri ya Madai - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Yaanza kuutangaza Mradi wa Mapitio ya Mfumo wa Utoaji Haki katika Mashauri ya Madai

Afisa Sheria Mkuu wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Anjela Shila (Kulia) akihojiwa na mtangazaji wa Kituo cha Radio 5 cha mkoani Arusha Devid Rwenyagira katika kipindi cha ‘Good Morning’  wakati wa kuutangaza Mradi wa Mapitio ya Mfumo wa Utoaji Haki katika Mashauri ya Madai.
 
Mkuu wa Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha Bw. Jowika Kasunga akipokea vipeperushi vinavyoelezea Mradi wa Mapitio ya Mfumo wa Utoaji Haki katika Mashauri ya Madai Tanzania kutoka kwa Afisa Sheria Mkuu wa Tume Anjela Shila ofisini kwake Wilayani Monduli mkoa wa Arusha.
 
Na Munir Shemweta, Arusha 

Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT) imeanza kuutangaza mradi wa Mapitio ya Mfumo wa Utoaji Haki katika Mashauri ya Madai nchini. 

  Katika hatua hiyo Maafisa Sheria wa Tume wameenda mikoa sita ya Tanzania Bara kwa ajili ya kuzungumzia mradi huo kupitia vituo vya Radio vilivyopo katika mikoa husika. 
 
Mbali na maafisa sheria kuzungumzia mradi huo katika vituo vya radio pia vipeperushi vinavyoelezea mradi wa Mapitio ya Mfumo wa Haki katika Mashauri ya Madai vimesambazwa katika wilaya zilizopo kwenye mikoa hiyo. 

Mikoa inayotembelewa Maafisa Sheria wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania ni Arusha, Mwanza, Dodoma, Iringa, Morogoro na Mtwara. 

Wakiwa katika mikoa hiyo Maafisa Sheria wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania wanaelezea hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Tume katika kuboresha mfumo mzima wa Utoaji Haki katika Mashauri ya Madai nchini Tanzania. 

Mradi wa Mapitio ya Sheria za Madai ni moja ya hatua zilizochukuliwa na Serikali ya Tanzania chini ya Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara Tanzania (BEST) ambao unalenga kuondoa vipingamizi vya kiuratibu na kiutawala katika kufanya biashara. 

Mapitio hayo yanalenga kuboresha Mfumo wa Utoaji Haki za Madai Tanzania ili kupunguza ucheleweshaji, gharama na ugumu wa utatuzi wa mashauri ya madai ili kuendana na ibara ya 107 A ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika mradi huo Sheria ya mwenrendo wa mashauri ya madai ni mojawapo ya sheria zinazofanyiwa kazi.  

Tume kupitia mradi huo inafanya mapitio ya kanuni zinazohusu Mfumo wa Haki za Madai tisa (9) zinazohusiana na uendeshaji wa mashauri ya madai. Kanuni hizo ni pamoja na zinazohusu Tozo za Ada za Mahakama, Likizo za Mahakama, Maafisa wa Serikali kuwakilisha Serikali Mahakamani, Tozo za Ada kwenye Mahakama kuu, kanuni zinazohusui Lugha ya Mahakama na kanuni za Maadili. 

Kanuni hizo zote ni changamoto zilizobainishwa na Tume baada ya kuzifanyia mapitio katika Mfumo wa Haki za Madai na zimefanyiwa kazi ili kutoa mapendekezo yatakayosaidia kuboresha mfumo wa utatuzi wa migogoro ya madai hapa nchini.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages