Kamati ya Ligi ya Vijana “Central Taifa” Zanzibar Yakutana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Kamati ya Ligi ya Vijana “Central Taifa” Zanzibar Yakutana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad

  Mwenyekiti wa baraza la michezo Taifa Bi Sherry Khamis akitoa ufafanuzi mbele ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad kuhusiana na mwendelezo wa ligi ya Central Taifa. Kushoto ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akisalimiana na baadhi ya wajumbe wa kamati ya ligi ya vijana “Central Taifa” waliofika ofisini kwake Migombani kwa ajili ya kubadilishana nae mawazo. Katikati ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk na pembeni (kulia) ni mwenyekiti wa Baraza la Michezo Zanzibar Bi Sherry Khamis.Picha na Salmin Said,Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar
--
Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Zanzibar imesema itafanya kila liwezekanalo ili kuiwezesha ligi ya vijana Zanzibar iweze kusonga mbele.

 Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Said Ali Mbarouk alitoa ahadi hiyo mbele ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, wakati kamati ya ligi hiyo Central Taifa ilipokutana na Maalim Seif ofisini kwake Migombani. 

 Aliahidi kuwa Wizara ya habari itatafuta fedha kwa njia yoyote ili kuhakikisha kuwa fainali za ligi hiyo inayotarajiwa kufikia kilele chake July mwaka huu kwa timu za Juvinail, Junior na Central zinafanikiwa. 

Alisema ligi hiyo ni muhimu katika kuibua vipaji vya vijana ambavyo vitasaidia kuinua soka la Zanzibar. Kwa upande wake Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad amewataka viongozi wa ligi hiyo kuwa na dhamira ya kweli katika kuendeleza ligi hiyo, sambamba na kuepukana na vitendo vyovyote vya udanganyifu katika kuibua vipaji vya wanasoka vijana. “Sisi serikali tuko very serious na mimi binafsi niko interested kuona hadhi ya michezo inarejea Zanzibar, kwa hiyo na nyinyi viongozi muwe serious kwa hili”, alisistiza Maalim Seif. 

 Amewatahadharisha viongozi hao kuzitumia fedha wanazopewa kwa kutimiza malengo yaliyokusudiwa na sio kuzitumia kwa maslahi binafsi. “ Wakati mwengine tunakosa ufadhili kwa kuwa hatuko serious, hao wafadhili nao wanaangalia ni kwa kiasi gani fedha zao zinatumika kwa malengo yanayokusudiwa, vyenginevyo ndio wanaona hakuna haja ya kutoa ufadhili” aliongeza. 

 Nao viongozi wa chama cha soka Zanzibar ZFA wakiwemo kaimu Rais wa ZFA Haji Ameir na mwenyekiti wa Baraza la Michezo Zanzibar Bi Sherry Khamis, wamesifu utendaji wa Waziri mpya wa Wizara hiyo Mhe. Said Ali Mbarouk, na kwamba unawapa changamoto katika utendaji wao. 

Wamesema Waziri huyo amedhamiria kweli kufanya kazi aliyotumwa na kamwe hakuna mzaha wala muhali, kama ambavyo mwenyewe amekuwa akieleza mara kwa mara. Ligi ya vijana kwa ngazi za Juvenile, Junior na Central inazishirikisha timu za mitaani za vijana zilizopata usajili ambazo hushindana hadi ngazi ya Wilaya Unguja na Pemba ambapo hupatikana mshindi mmoja kwa kila Wilaya, na kuanzia hapo ndio kamati ya Central Taifa hushughulikia kwa ajili ya kuandaa fainali ambazo hufanyika Unguja na Pemba.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages