MAKABIDHIANO YA MKOA MPYA WA KATAVI YAFANYIKA JANA, WENGI WAJITOKEZA KUWALAKI VIONGOZI WAO WAPYA NA KUFURAHIA KUPATA MKOA MPYA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

demo-image

MAKABIDHIANO YA MKOA MPYA WA KATAVI YAFANYIKA JANA, WENGI WAJITOKEZA KUWALAKI VIONGOZI WAO WAPYA NA KUFURAHIA KUPATA MKOA MPYA

DSC03165
Hapa ni Mpakani mwa Mikoa ya Rukwa na Katavi kwenye Mlima maarufu wa Lyamba Lyamfipa. Utawala wa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya unaishia hapa, anashusha kibendera kuruhusu Utawala Mpya wa Dkt. Rajab Mtumwa Rutengwe kupandisha bendera yake tayari kuipepeza kwenye Milima na Mabonde ya Utawala wake Mpya wa Mkoa Mpya wa Katavi.
DSC03168
Bendera ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya imeshashushwa.
DSC03167
Mkuu wa Mkoa Mpya wa Katavi Dkt. Rajab Mtumwa Rutengwe akiwa tayari kupepeza bendera yake kwa mara ya kwanza katika Mkoa wake mpya wa Katavi baada ya kukabidhiwa Mkoa huo jana.
DSC03062
Safari ya kuelekea makabidhiano ilianza ofisini kwa Mkuu wa Mkoa Rukwa Injinia Stella Manyanya ambaye alianza kwa kumuombea dua Mkuu wa Mkoa Mpya wa Katavi Dkt. Rajab Rutegwe mapema kabla ya kuanza safari kuelekea Wilayani Mpanda Mkoa Mpya wa Katavi ambapo ndipo yalipofanyika makabidhiano hayo. Mkoa wa Rukwa umegawa na kuundwa Mkoa Mpya wa Katavi ikiwa ni juhudi za Serikali katika kusogeza huduma zake kwa wananchi. Kwa pamoja viongozi wote wa Mikoa ya Rukwa na Katavi wameishukuru sana Serikali ya Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuugawa Mkoa wa Rukwa kwa maslahi ya wananchi wake.
DSC02499
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya katikati akiwatambulisha viongozi wapya wa Mkoa Mpya wa Katavi kwa wananchi wa Mkoa huo jana kwenye uwanja wa Kashaulili Wilayani Mpanda katika makabidhianao ya Mkoa huo baada ya uliokuwa Mkoa wa Rukwa kugawanywa ikiwa ni jitihada za Serikali kusogeza huduma kwa Wananchi wake. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Rajab Mtumwa Rutegwe na Katibu Tawala Injinia Emmanuel Kalobelo.
DSC03277
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akihutubia wananchi wa Mkoa Mpya wa Katavi waliojitokeza kwa wingi kabla ya kuwatambulisha viongozi wao katika uwanja wa Mpira wa Kashaulili uliopo Wilayani Mpanda. Aliwaomba wananchi hao kuwapa viongozi wao wapya ushirikiano wa dhati ili kurahisisha utendaji kazi wao kwa maendeleoa ya Katavi na Ukanda mzima wa Ziwa Tanganyika.
DSC03304
 Mkuu wa Mkoa Mpya wa Katavi Dkt. Rajab Mtumwa Rutengwe akihutubia wananchi wake wa Mkoa Mpya wa Katavi mara baada ya kutambulishwa kwao na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa. Aliwaahidi ushirikiano wa hali na mali kuhakikisha Katavi inasonga mbele.Picha na Habari Zimeletwa hapa na Hamza Temba - Afisa Habari Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa kwa habari zaidi Kuhusu Mkoa wa Rukwa Bofya Hapa...>>>>

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Pages