YANGA YALAMBISHWA LAMBALAMBA NA AZAM KWA KUPOKEA KICHAPO CHA MAGOLI 3 KWA 1 - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

YANGA YALAMBISHWA LAMBALAMBA NA AZAM KWA KUPOKEA KICHAPO CHA MAGOLI 3 KWA 1

 *Mchezo wageuka Ulingo kama Misri, Wachezaji wamkimbiza mwamuzi kama Kuku uwanjani. Pichani juu, ni kipa wa Yanga, Shaban Kado, akiokoa moja ya hatari zilizoelekezwa langoni kwake, wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kati ya Yanga na Azam, uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo jioni.
Katika mchezo huo Azam imeibuka na ushindi wa mabao 3-1, huku Yanga ikicheza pungufu wakiwa wachezaji 9 uwanjani baada ya wachezaji wawili, Haruna Niyonzima na Haroub Canavaro kupewa kadi katika kipindi cha kwanza cha mchezo kufuatia vurugu zilizotokea uwanjani hapo. 
 Mwamuzi wa mchezo huo, Israel Mongo, akitoka baruti 'Nduki' kuwakimbia wachezaji wa Yanga baada ya kutoa kadi mbili kwa wachezaji wa Yanga, jambo ambalo lilipingwa na wachezaji wa Yanga na kuzua mtafaruku uwanjani hapo.
 Tukio jingine lililowashangaza mashabiki wa Soka waliokuwapo uwanjani hapo ni tukio hili la Askari Polisi aliyetinga magwanda, ambaye alitinga katikati ya uwanja wakati waa vurugu hizo na kuamulia ugomvi, jambo ambalo lingeweza kuamsha hasira zaidi za mashabiki.Picha Na Sufiani Mafoto

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages