WANAFUNZI MLIMANI WAKUMBWA NA UGONJWA WA RED EYES - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

WANAFUNZI MLIMANI WAKUMBWA NA UGONJWA WA RED EYES

Ukumbi wa Nkurumah uliopo chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam.
...........
UGONJWA WA ‘’RED EYES’’ WAANZA KUTIKISA WANAJUMUYIA WA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM 

 MIWANI MYEUSI YAVALIWA KUSTIRI MACHO YA WAGONJWA

NANI ALAUMIWE UCHEREWESHWAJI WA PESA ZA KUJIKIMU ZA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU 
 
 UGUMU WA MAISHA WAENDELEA KUWA GUMZO  MITAANI NA MAOFISINI 
 
 KUMBE 90% YA WANAFUNZI WA UDSM WANATEGEMEA BOOM KUENDESHA MAISHA YAO


Ikiwa ni hali ya kawaida ya kila mwaka wakazi wa chuo kikuu cha Dar es salaam na maeneo jirani kukumbwa na ugonjwa wa macho maarufu kwa jina la RED EYES, Ugonjwa huo umerudi tena ambako wagonjwa mbalimbali wameripotiwa kuugua ugonjwa huo. Mlimani leo ilipiga kambi hospitali ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam na kujionea wagonjwa mbalimbali waliojitokeza kupatiwa tiba hiyo.Hata hivyo wengi wa wagonjwa walionekana wakiwa katika hali ya awali ya ukuaji wa ugonjwa huo kwani macho yao hayakuonekana kuwa mekundu sana na macho kuvimba kama ilivyo kawaida ya ugonjwa huo katika dalili zake.Mlimani leo ilimtafuta Mganga Mkuu wa Hospitali ya chuo hicho kueleza mwenendo mzima wa ugonjwa huo na pengine idadi ya wagonjwa waliofika katika hospitali hiyo kupatiwa matibabu ambako ilielezwa yakwamba alikuwa nje ya ofisi.Nao baadhi ya wagonjwa walioambukizwa na ugonjwa huo walionekana kuvaa miwani myeusi kusitiri macho yao mbele za watu.
 
MLIMANI LEO TUNAPENDA KUWAPA POLE WAGONJWA WOTE WALIOAMBUKIZWA NA UGONJWA HUO. AIDHA  TUNAPENDA KUWASHAURI WAKAZI WOTE WA CHUO KIKUU  CHA DAR ES SALAAM KUZINGATIA USAFI MARA KWA MARA, IKIWA NI PAMOJA NA KUNAWA KWA SABUNI,KUTOSHIKANA MIKONO NA MGONJWA AU KUSHIKA VYUMA/MBAO (‘’BALIKONZI’’) ZILIZOPO KANDO YA NGAZI ZILIZOPO KATIKA HOSTELI ZETU . KUTOKUMBATIANA NA MGOJWA ILI KUWEZA KUPUNGUZA MAAMBUKIZI HAYO. PAMOJA NA HAYO JAMBO HILO LIFANYWE KWA NIA NJEMA ISIJE KUONEKANA YAKUWA TUNAWATENGA WAGONJWA.


Ø NANI ALAUMIWE UCHEREWESHWAJI WA PESA ZA KUJIKIMU ZA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
 
Pamoja na serikali kujitahidi kutoa fedha za kujikimu kwa wanafunzi wa Elimu ya juu hususani Chuo Kikuu cha Dar es salaam mapema kabisa, Zamu hii hali ilikuwa tafauti kwa utoaji wa huduma hiyo. Hali ilikuwa ngumu kwa  wanafunzi  hususani wanaotegemea ‘boom’ ambao wengi wao walikuwa mitaani na wengine wakiwa wameenda makwao.Hili lilijidhihirisha juma la kwanza wakati chuo kimefunguliwa ambako hapakuwepo wanafunzi katika viunga vya udsm ingawa ni vigumu kusema hawakuwepo kabisa.Wanafunzi hawa wawe wa kike au wakiume wengi wao wanategemea ‘boom’, jambo ambalo liliwawia gumu kutoka makwao mikoani kwani wanategemea boom kwa mambo mengi,mambo hayo yanatofautiana baina ya mtu na mtu.Wapo wanao tunza wazazi wao,wanaojilipia ada wenyewe tena kwa asilimia kubwa, wapo waliokuwa wanategemea nauli itoke kwenye boom hilohilo,wapo wanaopanga mitaani ambako wanalazimika kulipa pango la nyumba tena kwa miezi sita,wapo wanao tunza wadogo zao kwani inawezekana katika familia mwanafunzi huyu ndiye wa kwanza mwenye uwezo wa aina hiyo.Kwa ujumla hadithi ni nyingi juu ya matumizi ya pesa hizi kulingana na mtu mwenyewe.Katika juma hilohilo la kwanza Mlimani leo ilishuhudia mambo kadha wa kadha.Kwanza hapakuwepo usajili wa wanafunzi na hii si kusema kwamba wahusika wa kutoa huduma hiyo hawakuwepo bali wakusajiliwa hawakuwepo. Pili ni juu ya jitihada zilizokuwa zinafanywa na uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam katika kufuatilia Stahiki za wanafunzi ambako ndugu Prof. Yunusu Mgaya alitoa taarifa kwa umma zaidi ya mara mbili kuwataka wanafunzi wawe watulivu,Kiongozi huyo alisema endapo pesa ikifikia hatua ya uwezo wa kimamlaka Uliyonayo chuo, kitatoa pesa hizo kwa wanafunzi. Tunafikiri Prof. lilikuwa jukumu lake kufanya hivyo kwa kuujulisha umma lakini pia inawezekana aling’atwa na nyoka katika semista ya kwanza kwa kushuhudia vurugu kubwa.Kwa hiyo alikuwa sahihi kumuona mjusi na kushtuka.


Pamoja na hayo cha kushangaza hata wafanyakazi wa chuo walicheleweshewa pesa zao kwa kutoingia kwa wakati.Na hili kuweka uwazi Prof. Mgaya aliambatanisha matangazo hayo mawili kwa pamoja kuonyesha tatizo si tu kwa wanafunzi bali hata kwa wafanyakazi wa chuo.Alichokuwa na imani Prof. mgaya ni kuwa wafanyakazi wasinge andamana mpaka utawala au kuitisha Rv.squre(Hawa wanakufa kimoyomoyo).
 
Mlimani leo tunayasema haya kwa nia njema kabisa, na ndipo inakuja hoja ya NANI ALAUMIWE.Je tumlaumu Rais Kikwete, Waziri wa Elimu Ndugu Kawambwa,Mkurugenzi wa Bodi ya Mikopo ndugu George Nyantega,Makamu Mkuu wa Chuo ndugu Prof. Mukandara,Ndugu Prof. Mgaya, Afisa Mikopo wa chuo ndugu Silivanus au Rais wa Daruso ndugu Kilawa Saimoni na Mawaziri wake husika.Mchawi yuko wapi katika hili?.Upo usemi ati kila mtanzania siku hizi analalamika, awe kiongozi au si kiongozi.Na sisi tunapenda kwa moyo mkunjufu kabisa tuwe watanzania wakwanza wanaolalamika kwa hili.
 
Wafanyakazi wa chuo kukosa mishahara yao kwa wakati siyo peke yao,wapo pia askari polisi walicheleweshewa pesa zao,walimu nao walikuwa katika orodha hiyo, wapo pia mabalozi wanao wakilisha nchi yetu nao walicheleweshewa pesa yao ingawa hapa Ikulu ilikanusha jambo hili.
 
Je hapa mchawi ni Prof. Mgaya au Mh, Rais .Je ni kweli tukisema tuilamu BODI ya Mikopo,hiyo bodi inahusika kutoa mishara ya wafanyakazi.Je mamlaka ya chuo katika kufuatilia stahiki za watu wake zinaishia wapi.Kama kweli mishahara na posho za wanafunzi zinacheleweshwa kwa sababu tuna watumishi wavivu hasa hapa kwetu ni dhahiri wawajibishwe kwa mujibu wa sheria,Kama tuna viongozi wa Daruso wanaopendelea kuitwa waheshimiwa bila kufanya kazi nao hawatufai,Kama pesa zinaingia kwenye akaunti ya chuo zinapangiwa shughuli nyingine nao pia viongozi wa aina hiyo hawatufai.Kama tunanunua mashangingi makubwa ya zaidi ya milioni 200, tunaagiza maua na meza za ofisini nje ya nchi tunategemea nini.Na anayeagiza hapa si Kikwete ni watumishi wa sekta husika.Makongamano na warsha haziishi.
 
Mkurugenzi badala ya kwenda peke yake kwenye semina analazimika kuondoka na msafara, mwisho wa siku tunafikia hatua ya kukopa Benki ya Standard charted au Exim  Bank ili tuwalipe mishahara wafanyakazi. Matumizi yanakuwa makubwa mno zaidi ya kile tunachoingiza.Je sisi na wewe tuko upande gani. Ndugu yetu ambaye hujaajiriwa umejipangaje  na hili.Je tunachambua mfumo mzima wa utoaji fedha na kuridhika nao,je ni endelevu na utakomboa vizazi vijavyo. TUNAOMBA KUTOA HOJA!!
 
Tukutane Toleo Lijalo,Kwetu Pakavu Tutilie Mchuzi.
MHARIRI MKUU 0718732487 E-mail athumanidrisa@rocketmail.com, MHARIRI MKUU MSAIDIZI +255718169191  E-mail anthonlouismwangake@rocketmail.com

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages