Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Akabidhi Vikundi Vya Wanawake Zanzibar Nyenzo za kazi. - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Akabidhi Vikundi Vya Wanawake Zanzibar Nyenzo za kazi.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, akitowa nasaha zake kwa Wanawake  Wanavikundi wa Jimbo la Malindi wakati walipofika kutowa vifaa vya kujiendeleza vilivyotolewa na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Shein na Mke wa Makamu wa Pili wa Rais Mama Asha Balozi Seif, makabidhiano hayo yamefanyika katika Tawi la CCM Malindi. 
Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Balozi Seif Iddi, akitowa nasaha zake kwa Wanawake wa Vikundi vya jimbo la Mtoni katika tawi la CCM Mtoni, na kuwataka wasiwe wakiwa kwa kutokuwa na mbunge na mwakilishi wa CCM katika jimbo hilo kwani wao ndio walezi wao mna wako tayari kutowa msaada wakati wowote wakiwa na shinda katika vikundi vyao.   
Katibu wa Wake wa Wawakilishi na Wabunge Zufura Mgeni Mwalim akisoma majina ya Wanavikundi ili kukabidhiwa vifaa vyao kwa ajili ya kuzalisha mali katika vikundi hivyo ili kujiegezea kipato katika kazi za amali.
Mwenyekiti wa UWT Jimbo la Mji Mkongwe Fatma Hamza akitowa neno la shukrani kwa msaada waliopata kwa vikundi vya jimbo lao baada ya makabidhiano hayo yaliofanyika tawi la CCM Malindi.
Khadija Seif akisoma risala kwa niaba ya Wanawake wa Jimbo la Malindi wakati wa hafla ya kukabidhiwa vitendea kazi kwa vikundi vya Wanawake wa Jimbo hilo zilizofanyika katika tawi la CCM Malindi.
Wanawake wa Viongozi wakisikiliza Makamu wa Pili wa Rais akitowa nasaha zake kwa Wanavikundi wa Mji mkongwe baada ya kukabidhi vitendea kazi vya vikundi hivyo, vilivyotolewa na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Shein na Mke wa Makamu wa Pili Mama Asha Balozi Seif kwa vikundi hivyo kujiendeleza kiuchumi na kujiogezea kipato chao. 

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages