KAMPUNI YA BIA YA SERENGETI KUJENGA MRADI WA UVUNAJI MAJI HOSPITALI YA WILAYA IRINGA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

KAMPUNI YA BIA YA SERENGETI KUJENGA MRADI WA UVUNAJI MAJI HOSPITALI YA WILAYA IRINGA

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL)Teddy Mapunda kulia akisalimiana na Galus Lugenge Diwani wa kata ya Mwangata Frelimo, wakati alipotembelea Hospitali ya Wilaya ya Iringa mjini kwa ajili ya ukaguzi wa ujenzi wa mradi wa uvunaji maji hospitalini hapo, anayefuatia ni Nandi Mwiyombela Meneja wa Miradi Endelevu na Uwajibikaji (SBL), Caroli Lunyili Injinia wa maji Manispaa ya Iringa na kushoto ni Stella Kiwele Mganga mkuu msaidizi wa Hospitali ya Wilaya Iringa. Mradi huo utagharimu kiasi cha shilingi milioni 20 na unatarajiwa kusaidia watu zaidi ya 150.000 katika manispaa hiyo wanaozunguka eneo la Hospitali.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya bia ya Serengeti SBL Teddy Mapunda akisaini kitabu cha wageni wakati alipowasili hospitalini hapo tayari kwa ukaguzi wa mradi wa Uvunaji maji unaojengwa katika hospitali hiyo, kulia ni Mwenyeji wake Stella Kiwele Mganga Mkuu msaidizi wa Hospitali ya Wilaya Iringa, na kushoto ni Nandi Mwiyombela Meneja wa Miradi Endelevu na Uwajibikaji.
Na haya ndiyo majengo ya Hospitali hiyo yanavyoonekana.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages