
Waziri
Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba (kulia) akipata maelezo kutoka
kwa Afisa Masoko Mwandamizi wa Mfuko wa Akiba ya Wafanyakazi Serikalini
(GEPF) James Mlowe (kushoto) juu ya majukumu ya mfuko huo
na faida za kujiunga kwa wananchi. Waziri Mkuu huyo alipata maelezo hayo
jana jijini Dar es salaam alipotembelea banda la Wizara ya Fedha wakati
wa maonyesho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara yanayoendelea katika
Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Mchambuzi
wa Mifumo ya Kompyuta kutoka Idara ya Usimamizi wa Mifumo ya Fedha
Wizara ya Fedha Elimu Sekeni (katikati) akitoa ufafanuzi kwa Waziri Mkuu
Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba (kulia) juu ya majukumu ya Idara hiyo
. Waziri Mkuu huyo alipata maelezo hayo jana jijini Dar es salaam
alipotembelea banda la Wizara ya Fedha wakati wa maonyesho ya miaka 50
ya Uhuru wa Tanzania Bara yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu
Julius Kambarage Nyerere

Waziri
Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba (kushoto) akipata maelezo kutoka
kwa Maafisa wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu(NBAA)
juu ya mafunzo mbalimbali yanayotolewa na Bodi katika kuimarisha taaluma
ya ugavi na uhasibu nchini. Waziri Mkuu huyo alipata maelezo hayo jana
jijini Dar es salaam alipotembelea banda la Wizara ya Fedha wakati wa
maonyesho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara yanayoendelea katika
Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Afisa
Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Simoni
Masawe(kulia) akitoa ufafanuzi kwa Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde
Warioba (kushoto) juu ya jitihada mbalimbali zinazotumiwa na Mamlaka
hiyo katika kuwaelimisha wafanyabiashara juu ya umuhimu wa kulipa kodi .
Waziri Mkuu huyo alipata maelezo hayo jana jijini Dar es salaam
alipotembelea banda la Wizara ya Fedha wakati wa maonyesho ya miaka 50
ya Uhuru wa Tanzania Bara yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu
Julius Kambarage Nyerere.

Waziri
Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba (kushoto) akiangalia machapisho
mbalimbali ya Benki ya Uwekezaji Tanzania (TIB) yanayoonyesha fursa
mbalimbali ambazo mwananchi anaweza kuzipata kupitia Benki hiyo katika
kujikomboa kiuchumi. Waziri Mkuu huyo alipata maelezo hayo
jana jijini Dar es salaam alipotembelea banda la Wizara ya Fedha wakati
wa maonyesho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara yanayoendelea katika
Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.Picha na Tiganya Vincent- MAELEZO--Dar es salaam

No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)