TASWIRA ZA MJI WA KAMACHUMU WILAYA YA MULEBA MKOANI KAGERA KAMA ZILIVYOTUFIKIA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

TASWIRA ZA MJI WA KAMACHUMU WILAYA YA MULEBA MKOANI KAGERA KAMA ZILIVYOTUFIKIA

Katika pita pita zangu hii leo nikiwa anga za kamachumu km 2 kabla ya kuingia mjini Milama,Nalazimika kufika kwenye nyumba ya mushonge nipati walau picha na uhalisia wa ndani.
Nyumba ipo katikati ya shamba zuri la migomba yenye afya!!!
Ikiwa kwenye mazingira safi imewekewa uzio wa matete(embingo kama wasemavyo wao)nakumbuka enzi hizo matete yakitengeneza vitanda vya kulalia binafsi nimepitia maisha hayo.
Baadhi ya viunga vya Kamachumu hii leo.
Yaap moja kwa moja nakanyaga kwenye mji wa Kamachumu,Mji wenye hekaheka nyingi,wadau wengi ni watata sana,Mji huu ndiyo chimbuko la maaskofu wakubwa na maarufu tukianza na Askofi Kibila na hapo hapo anazaliwa Cardinal wa kwanza wa Afrika Cardinal Laurean Rugambwa

Watu maarufu walitokea hapo akina Anthony Rugangila,Kalinjuma,na Ntonini,Haji Hamad,Byabusha,Mzee Songoro aka Karasha,familia ya Bukenya alikadhalika Zakalia Mugyabuso Petro Nshange aka (kibunda) na Christopha Ngaiza wote ni marehemu
Majemedali wengi kama bora Imani,Haji Birundulu na Haji Kabalala,Mzee Kabea na Haji Hamad nitakua sijatenda haki nisipo mkumbuka Bandeko na familia nzima ya akina Fresh.

Pia ipo familia ya al-squar ndio akina mawingu ,Adara na wadau wengine wengi hii ni kwa mkutasari tu!!!

Kwa sasa wapo akina Hamed Kiwanuka ,Haji Jaffary, Veda Rugabela,Mdau Myaga , Mzee Thadeo Iluganyuma na Mdau Sued ukanda wa Rutabo akiwepo Mzee Nestory Kato, mdau Chamisili na mwalimu Mastura.Picha Na Mdau Mc Baraka Wa Bukoba Wadau

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages