Wizara
ya Nishati na Madini
ikishirikiana na ubalozi wa Tanzania Uk wameandaa kongamano la
uwekezaji nchini. Hii ni katika kutekeleza sera za economic diplomacy
pamoja na kuvutia mitaji ya kigeni. Mada nyingi zilizungumziwa kuhusu
nafasi na sheria za uwekezaji Tanzania. Waziri Ngeleja kama mgeni rasmi
na mwakilishi wa taifa aliwawekea wazi wawekezaji jinsi ya sheria mpya
zilizotungwa na kuwahakikishia kuwa Tanzania na Watanzania wako tayari
kupokea wawekezaji ambao wako tayari kuwekeza ilimradi waje na njia
ambazo hazitinyinya Watanzania na taifa lao.
Eneo
lililovutia sana washiriki lilikuwa eneo la
nishati na madini pamija na viwanda. Waekezaji ambao tayari wako
nymbanu Tanzania wamwisifia sana kwamb kwasasa Tanzania inawezekana kuwa
ndio nchi pekeweafrika yenye mazingira sawia kwa wawekezaji toka nje.
Wanataaluma nao kama bi Barbara Njau alifafanua kwa ushahidi wa
vielelezo kuwa uchumi Watanzania siku zijazo utakuwa haraka sana na
yakuwa Watanzania na Tanzania wako kwenye nafasi nzuri kabisa
kimaendeleo kama watatumia rasilimali walizonazo kwa umakini na
uangalifu.
Mh Ngeleja akitoa maelezo juu ya sheria mpya za uwekezaji kwenye eneo la nishati
Mh ngeleja akibadilishana mawzo na Naibu Balozi chabaka na Moja ya wanakongamano
Waziri Ngeleja akiwa na Wajumbe wa JumuiyaTanzanian Uk





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)