MR. EBBO KUZIKWA KESHO JIJINI ARUSHA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

MR. EBBO KUZIKWA KESHO JIJINI ARUSHA


NA GLADNESS MUSHI WA FULLSHANGWE- ARUSHA
 
MSANII wa kizazi kipya Abel Motika maarufu Mr Ebo(37) aliyefariki desemba Mosi mwaka huu saa 4.30, katika hospitali ya misheni(Dream) iliyopo Usa River wilayani Arumeru ,anazikwa leo jumatatu katika shamba la baba yake mzazi eneo la Kijenge chini ,manispaa ya Arusha.
Mazishi hayo yanatarajiwa kuvuta umati mkubwa wa wakazi wa maeneo mbalimbali nchini wakiwemo mashuhuri na tayari wageni mbalimbali wameingia kushiriki mazishi hayo ,ambapo pia wasanii mbalimbali kutoka Mkoani Tanga,Dar es salaam na mikoa mingine jirani wanataarajiwa kuhudhulia mazishi hayo.

Kwa mujibu wa msemaji wa familia ya Mzee Motika ,ambaye ni kaka mkubwa wa marehemu Mr Ebo,Olais Motika(58) alisema kuwa mazishi hayo yanatanguliwa na misa maalumu ya kuuombea mwili wa merehemu katika kanisa la Luthelani ,lililopo kata ya Olorien.

Alisema kuwa marehemu Ebo alikuwa mtoto wa 10 kati ya watoto 11 wa mzee Loshilaa Motika(85)ambapo kati yao wawili ni marehemu akiwemo Mr Ebo na kwamba marehemu alioa na kuzaa watoto watatu .
Alisema katika familia yao yeye Olais ni mtoto wa kwanza na kufuatiwa na Sion,John,Michael,Rose(marehemu) Ana,Kesia,Grace ,Imanuel ,Mr Ebo(marehemu) na Jackon ambaye ni mtoto wa mwisho.

Akisimulia zaidi , alisema kuwa marehemu alianza kuugua maradhi mbalimbali miezi mitano iliyopita na kutibiwa katika hospitali mbalimbali hapa nchini, ikiwemo hospitali ya rufaa ya KCMC iliyopo mkoani Kilimanjaro.

Aidha alisema awali marehemu Mr Ebo alikuwa akiishi Kisosora mkoani Tanga na kufanya shughuli zake mkoani humo baada ya kujenga nyumba yake kubwa na kufungua studio aliyokuwa akiimiliki na kurekodi nyimbo mbalimbali za wasanii wa mziki.

Aliongeza kuwa usanii alianza mwaka 2001 baada ya kutoa nyimbo yake ya ‘mimi mmasai bana’ hatua ambayo iliwashangaza familia yake lakini akadai kwamba walifurahia kazi yake kwa kuwa ilichangia kwa kiasi kikubwa kuitangaza familia ya mzee Motika na kufanya jina la Motika lijulikane .

Alifafanua kwamba baada ya kuugua na kuzidiwa alilazwa katika hospitali hiyo ya misheni na kwa mujibu wa waunguzi wa hospitali hiyo walieleza kwamba hali ya Mr. Ebo Ilikuwa ikibadilika mara kwa mara hadi desemba mosi majira ya saa 4.30 usiku alipofariki dunia baada ya hali yake kuwa mbaya zaidi.

Nae baba mzazi wa marehemu Mr Ebo,Mzee Loshinaa alisema kuwa amesikitishwa sana na kifo cha marehemu mwanae kwa kuwa hakutegemea kwamba ipo siku mwanae huyo aliyeipaisha familia yao angemtangulia ,hata hivyo ameiomba jamii kumwombea kwani mungu ametwaa na jina la bwana lihimidiwe.

Marehemu Mr Ebo ameacha mke,aliyetajwa kwa jina la Baby Shoo ,watoto watatu ambao ni Ashrey ,Adella na Alisha na wawili kati yao wanasoma nchini Uganda na watakuwepo kwenye mazishi ya baba yao ,pia marehemu ameacha vitu mbalimbali ikiwemo nyumba iliyopo mkoani Tanga na Studio ya kurekodi mziki.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages