Vick
Kamata amewaeleza wasanii mbalimbai waliohudhuria katika uzinduzi huo
kuwa anaimani kuwa sheria mpya ya haki miliki itatungwa na Bunge ili
kulinda kazi za wasanii kutokana na kuibiwa kazi zao muda mrefu.
Ameongeza kwamba kazi ya sanaa ni kazi nzuri ambayo imekuwa ikiwasaidia
wasanii kuishi maisha mazuri, lakini pia kufanya maendeleo katika
maisha yao.
Vick
Kamata amezindua filamu hiyo kwa niaba ya Waziri Mathias Chikawe
ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo hata hivyo
hakuhudhuria kutokana na majukumu mengine ya kitaifa
Eddie
Hanspoppe mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya Papa Zii akizungumza
katika uzinduzi huo, ambapo amewashukuru wageni waalikwa wote
waliohudhuria katika uzinduzi huo, akisema wameonyesha kwamba wamesikia
wito wa kampuni ya Papa Zii, na ameahidi kuwa kampuni hiyo itatekeleza
na kusimamia vyema kazi za wasanii hapa nchini.
Mkurugenzi
wa Masoko wa Kampuni ya Papaa Zii Vivian Sirikwa akizungumza katika
uzinduzi huo na kuelezea malengo ya kampuni hiyo, katika kukuza sanaa
na kuendeleza wasanii hapa nchini.
Steve
Mengele aka Steve Nyerere akitambulisha waigizaji wenzake
walioshiriki katika filamu ya Mr. President ambayo yeye mwenyewe
ameigiza kama Rais katika filamu hiyo, huku waigizaji wenzake wakonekana
wenye furaha katikauzinduzi huo.
Wsanii mbalimbali walioshiriki kuigiza filamu ya Mr. President wakiwa katika picha ya pamoja katika uzinduzi huo.
Mkurugenzi wa Masoko wa Papa Zii Vivian akiwa katika picha ya pamoja na Kaimu Balozi wa Palestine Derar Ghannam.
Peter John Lugabandana akiongea katika hafla hiyo ya uzinduzi na kukaribisha wageni mbalimbali.
Bendi ya Borabora Sound ikitumbuiza katika uzinduzi huo kwenye hoteli ya Serena Dar es salaam.
Vick
Kamata kulia mgeni rasmi katika uzinduzi wa Filamu ya Mr. President
iliyoandaliwa na kampuni ya Papa Zii unaofanyika usiku huu kwenye hoteli
Serena Dar es salaam usiku huu, ambapo wageni waalikwa mbalimbali
wameweza kufika katika uzinduzi huo ili kushuhudia kitakachojili kwenye
uzinduzi huo, katikati ni Mbunge wa Mbinga Magharibi Kpt. John Komba na kulia ni Benny Kinyaiya.
Wazee
wa mpira kutoka kulia ni Evans Aveva akiongea na Charles Hamka,
Mohamed Nasor, Philemon pamoja na Juma Pinto wakishiriki katika
uzinduzi huo.
Wageni waalikwa mbalimbali wakiwa katika uzinduzi huo.
Kutoka kulia ni mtu mzima John Kitime, Rich Mtambalike na wapili kutoka kulia ni Cloud pamoja na marafiki zao.
Richard Mzirai pamoja na Mr Bandawe wakiwa katika uzinduzi huo kama wanavyoonekana.
Wadau Hamatton Bhao kulia na Rupe Mohamed wakishuhudia uzinduzi huo.
Wageni mbalimbali wakiwa katika uzinduzi wa filamu hiyo. 




No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)