Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Mohammed Aboud Mohammed
--
NA HABARI MAELEZO ZANZIBAR
Jumla
ya Shl.Bilioni 1 na Millioni 100 zimekusanywa na Kamati ya Taifa ya
Maafa Zanzibar hadi kufikia leo ikiwa ni michango mbalimbali kutoka kwa
Taasisi,Watu binafsi na Wadau mbalimbali wa nje na ndani ya Zanzibar
kutokana na ajali ya Meli ya Mv. Spice Islanders.
Hayo
yameelezwa hivi leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais
Mohammed Aboud Mohammed huko ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar wakati
alipokuwa akipokea Mchango wa Dola za Kimarekani 1444 sawa na Shl.
Milioni 2 laki Moja na Hamsini na Nne na Mia Nane kutoka kwa Watafiti
mbalimbali kutoka nje.
Waziri
Aboud amesema kuwa Serikali imefarijika sana kutokana na wanafunzi hao
kuona umuhimu wa kutoa michango hiyo kwa waathirika wa ajali hiyo ya
Meli ya Mv. Spice Islanders.Amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
hadi sasa bado haijatumia fedha yoyote ile iliyotolewa kwa Michango hiyo
ambapo fedha hizo zinatarajiwa kutolewa mara tu Tume ya Uchunguzi ya
Ajali hiyo iliyoteuliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi kutoa taarifa yake.
Akikabidhi
mchango huo kwa niaba ya Watafiti hao Dk. Naiman Saleh Jidawi ambaye ni
Mkuu wa Chuo cha Sayansi ya Baharini Zanzibar kilichopo chini ya Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam amesema kuwa wanafunzi hao wameguswa sana na
ajali hiyo hivyo wameona na wao watoe mchango wao.
Aidha
amesema kuwa Fedha hizo walizochangia zitasaidi katika malengo
yaliyokusudiwa kutekelezwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.Amesema
kuwa watafiti hao kutoka nje walishtushwa sana na tukio la ajali ya Mv.
Spice Islandes hivyo ikawalazimu kujikusanya pamoja na kuona kuwa wao
hawatajisikia vizuri ikiwa hawatochangia chochote kuhusiana na ajali
hiyo ambayo siyo ya Zanzibar tu bali ni ya Tanzania kwa ujumla.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)