Wanamuziki
wa Bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' wakiwa Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo Alfajiri
wakati wakiondoka nchini kuelekea Uingereza ambao wanakwenda kufanya
maonyesho kadhaa, ambapo onyesho lao la kwanza linatarajia kuanza kesho
jijini humo.
********************************
Twanga
Pepeta ''KISIMA CHA BURUDANI'' wameondoka leo asubuhi kutoka uwanja wa
kimataifa wa Julius Nyerere wakienda kuwasugulisha Kisigino wapenzi wao
walioko katika Jiji la London nchini Uingereza na nchi jirani ikiwa ni
katika kusherehekea maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania.
Kundi
hilo lililokamilika katika safu zake za waimbaji, wapiga vyombo na
wacheza show linatarajiwa kuwasha moto wa burudani yao siku ya Jumamosi,
tarehe 26 Novemba 2011 katika Ukumbi wa Club 2000 Savoir Banqueting
Suite, Popin Building Southway, Wembley HA9 0HB kuanzia saa Tatu Kamili
Usiku mpaka alfajiri (9pm til late).
Mheshimiwa
Balozi Peter Kalaghe atakuwa mgeni rasmi. CD za album mpya na za zamani
zitauzwa na vinywaji pamoja na vyakula vya kitanzania vitakuwepo vya
kumwaga. Viingilio vitakuwa £20 (singles) na £35 (couples) kabla ya saa
sita (mid night) na £25 (singles) na £40 (couples) baada ya saa sita
usiku.
Njoo
tujumuike, njoo usugue kisigino, njoo usherehekee uhuru wa nchi yako,
njoo ule na kunywa kitanzania. Burudani ni watu na watu ni pamoja na
wewe. Tanzania itajengwa na watu wenye moyo kama wewe. Karibuni sana.
Kiongozi wa bendi hiyo, Charls Baba (katikati) akipozi na mpiga solo wake, Shakashia pamoja na Mnenguaji, Shalapova.
Mpiga Kinanda wa Bendi hiyo, Victor Mkambi akipozi na Mnenguaji, Maria Soloma.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)