Mgonjwa aliyezinduka akiwa Mochwari akihudumiwa na madaktari.
Na Francis Godwin, Iringa
Na Francis Godwin, Iringa
MAUZAUZA ya
amini usiamini yametokea mjini Iringa jana baada ya mgonjwa ambaye
alifika kufanyiwa maombi kwa mmoja kati ya wahubiri maarufu mkoani
Iringa kukata kauli akiwa nje ya ukumbi huo maarufu wa maombi na
kuonyesha dalili zote za kuaga dunia jambo lililowafanya walioongozana
naye kumpeleka kumuhifadhi katika chumba cha kuhifadhia maiti
(Mochwari) katika hospital ya mkoa wa Iringa.
Baada
ya kufikishwa katika Chumba hicho maiti hiyo iliamka ghafla na kukaa
ndipo wanandugu walipoamua kubeba mwili huo na kupeleka kwa madaktari
kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mke wa mgonjwa huyo, Amina Ramadhan, alisema kuwa mume wake alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa malaria kwa kipindi cha mwezi mmoja sasa kabla ya jana mgonjwa huyo kuomba kuletwa mjini Iringa kwa mhubiri huyo maarufu mkoani Iringa, Boaz Sollo, wa kituo cha maombezi cha overcomers .
Hata hivyo alisema kuwa akiwa katika foleni ya kuingia ndani ya ukumbi ghafla mgonjwa huyo aliomba kupelekwa chooni na kabla ya kuingia chooni alikata kauli na hivyo kulazimika kuupeleka mwili wake mochwari katika hospital ya mkoa ambako kabla ya kuingizwa Mochwari ghafla marehemu aliamka na kuanza kurusha rusha mikono yake hali iliyopelekea kurudishwa tena mapokezi kwa ajili ya kuchunguzwa zaidi na kumtaja mjane wa marehemu Bi Amina Ramadhan alimtaja marehemu kuwa ni Gerald Tadei Ngusi.
Tukio hili limetokea majira ya saa 10 za jioni katika ukumbi huo wa IDYDC mjini Iringa madaktari walikwisha mpima na kuthibitisha kifo cha mgonjwa huyo.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mke wa mgonjwa huyo, Amina Ramadhan, alisema kuwa mume wake alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa malaria kwa kipindi cha mwezi mmoja sasa kabla ya jana mgonjwa huyo kuomba kuletwa mjini Iringa kwa mhubiri huyo maarufu mkoani Iringa, Boaz Sollo, wa kituo cha maombezi cha overcomers .
Hata hivyo alisema kuwa akiwa katika foleni ya kuingia ndani ya ukumbi ghafla mgonjwa huyo aliomba kupelekwa chooni na kabla ya kuingia chooni alikata kauli na hivyo kulazimika kuupeleka mwili wake mochwari katika hospital ya mkoa ambako kabla ya kuingizwa Mochwari ghafla marehemu aliamka na kuanza kurusha rusha mikono yake hali iliyopelekea kurudishwa tena mapokezi kwa ajili ya kuchunguzwa zaidi na kumtaja mjane wa marehemu Bi Amina Ramadhan alimtaja marehemu kuwa ni Gerald Tadei Ngusi.
Tukio hili limetokea majira ya saa 10 za jioni katika ukumbi huo wa IDYDC mjini Iringa madaktari walikwisha mpima na kuthibitisha kifo cha mgonjwa huyo.
Wasamaliawema
wakimshusha kutoka kwenye gari mgonjwa huyo 'marehemu' ili kumuingiza
katika chumba cha matibabu baada ya kuzinduka akiwa Mochwari.
Wasamaria wema wakisimama nje ya chumba cha daktari kusubiri majibu huku mke wa marehemu akiwa amekaa chini.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)