Mratibu
wa tamasha la SIFA ZIVUME,pichani kulia,Mchungaji Safari akifafanua
jambo mbele ya Wanahabari kuhusiana na tamasha hilo,linalotarajiwa
kufanyika jumapili katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini.
DarMchungaji Safari amesema kuwa katika tamasha hilo kiingilio
kimepangwa kuwa ni 5000 kwa viti vya kawaida na shilingi 10,000 kwa
viti maalum,aidha ameongeza kuwa tiketi hizo zinapatikana DPC
Kinondoni,Mlimani City,Silva Spoon,Mwenge Christian Bookshop,CLC
Bookshop mtaa wa Mkwepu,Mbogo Shop Kariakoo na Mars Collection karibu
na Posta ya zamani.
Mchungaji Safari alibainisha kuwa mbali ya kundi hilo pia kutakuwepo
na makunndi mengine yatakayotumbuiza kama vile The Voice,Brother
Joshua,Victor Aron na Faith Sigers,Safari ameongeza kuwa pia
kutakuwepo na maombi ya kumshukuru Mungu kwa kufikisha miaka hamsini
ya Uhuru,
Pichani
ni baadhi ya waimbaji wa kundi la nyimbo za Injili la Rivers of Live
mbele ya Waandishi wa habari (hawapo Pichani),wakiimba akapera mara
baada ya kumaliza mkutano wao kuhusiana na tamasha lao litakaloitwa
SIFA ZIVUME,la kumsifu na kumuabudu Mungu,tamasha hilo ambalo
litaendana sambamba na uzinduzi wa DVD SIFA ZIVUME ambayo ina ujumbe wa
kubadili maisha ya watu na kuwapa tumaini,imerekodiwa kwa ubora wa
hali ya juu ili kufikia viwango vya Kimataifa,ina urefu wa masaa matatu
na inamesheheni nyimbo15
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)