Mwenyekiti wa Chama
cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. Jakaya Kikwete (kulia), akifungua rasmi
Kikao cha Kamati Kuu ya CCM, mjini Dodoma leo, ambacho kinatarajia
kumalizika kesho. Kutoka kushoto ni Wajumbe wa kudumu wa Kamati Kuu
hiyo, Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu, Benjamini Mkapa, Rais wa Zanzibar,
Dkt. Ali Mohamed Shein na Rais Mstaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM,
wakijisomea kabla ya kuanza kwa kikao hicho kilichofunguliwa na
Mwenyekiti wake Rais Jakaya Kikwete leo mjini Dodoma.
Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Waziri Mkuu Mstaafu,
Edward Lowasa akisalimiana na Mohamed Dewji, wakati walipokutana ndani
ya Ukumbi huo mjini Dodom leo Nevemba 23 wakati wa ufunguzi wa Mkutano
wa Kamati Kuu ya CCM.
Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Nape Nnauye na
Asha Baraka, wakisalimiana wakati walipokutana ndani ya ukumbi huo leo
mjini Dodoma.
Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Waziri Mkuu Mstaafu,
Fredrick Sumaye, akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu,
Edward Lowasa, wakati walipokutana ndani ya Ukumbi wa Makao Makuu ya CCM
mjini Dodoma leo.
Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Waziri Mku Mstaafu,
Fredrick Sumaye, akisalimiana na Nape Nnauye.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)