Mwenyekiti
wa chama cha demokrasi na maendeleo (Chadema),Freeman Mbowe akiwasili
kwenye Ofisi za Jeshi la Polisi Mkoani Arusha leo asubuhi kwa ajili ya
kujisalimisha kufuatiwa kusakwa na Jeshi hilo kwa tuhuma za kuvunja
sheria.
Mwenyekiti
wa Chadema,Freeman Mbowe akiingia katika ofisi za mkoa za Jeshi la
Polisi mkoni Arusha leo,aliyevaa nguo nyeusi ni Mbunge wa Viti Maalumu
wa Chadema,Joyce Mukya akiwa amemsindikiza mwenyekiti wao kujisalimisha
Polisi.
Mkuu
wa Operation wa Jeshi la Polisi Mkoani Arusha,Saimon Pilo (kulia)
akiwa amempokea Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe (katikati) katika
Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha kwa ajili ya kufanya nae
Mazungumzo,wakati Mwenyekiti huyo alipofika Kituoni hapo Kujisalimisha
leo asubuhi.Kushoto ni Mbunge wa Viti Maalumu wa Chadema,Joyce Mukya
alieongozana na Mwenyekiti wake.
Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe akiwa anatafakari jambo ndani ya Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa Arusha leo.
Mwenyekiti
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),Freeman Mbowe akitoka
kwenye Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha na kuelekea katika
Ofisi ya Upelelezi Wilaya ambapo alielekezwa aende huko na Mkuu wa
Operesheni wa Jeshi la Polisi Mkoani Arusha. Picha zote na Woinde Shizza,Arusha.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)