Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania
Bw.Rene Meza akiongea na wajumbe wa Jukwaa
la wahariri wa vyombo vya habari wakati mkurugenzi huyo alipokwenda
kujitambulisha ,kushoto Mwenyekiti wa Jukwaa la wahariri
Absalom Kibanda,na katikati ni Ofisa Mkuu wa
Masoko na Uhusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba
Mwenyekiti wa Jukwaa la wahariri Absalom
Kibanda akimtambulisha Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania
Bw.Rene Meza kushoto, kwa wahariri wakuu wa vyombo vya habari nchini
Tanzania,wakati mkurugenzi huyo alipokwenda kujitambulisha kwenye
mkutano wa Jukwaa la wahariri jijini Dares Salaam jana,katikati ni
Ofisa Mkuu wa Masoko na Uhusiano Mwamvita Makamba.
Baadhi ya wajumbe wa jukwaa la wahariri
wa habari wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Rene
Meza hayupo pichani alipokuwa akiongea nao wakati wa kujitambulisha kwa
jukwaa hilo.
Mkuu wa kitengo cha Mahusiano wa Vodacom
Tanzania Nector Pendael,akiwaelekeza baadhi ya wahariri wa vyombo vya
habari namna ya kutumia Webbox inayounganishwa kwenye Luninga na kutoa
huduma ya mtandao wakati mkurugenzi mtendaji wa
Vodacom Tanzania Rene Meza alipokwenda kujitambulisha
kwenye mkutano wa jukwaa la wahariri jijini Dares Salaam
jana.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Rene
Meza kulia akiwaangalia Ofisa Mkuu wa Masoko na Uhusiano Tanzania
Mwamvita Makamba katikati akisalimiana na mjumbe wa jukwaa
la wahariri Masoud Sanani wakati mkurugenzi huyo alipokwenda
kujitambulisha kwenye mkutano wa jukwaa la wahariri jijini
Dares Salaam jana.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)