Baadhi
ya wafanyabiashara wadogo wadogo wa mitaani (Wamachinga) wakijiandaa
kupambana na askari wa kutuliza ghasia (FFU) walipokuwa wakitawanywa na
askari hao wakati walipofika katika Ofisi za Kata ya Sinde na Uyole kwa
lengo la kuziharibu ofisi hizo kwa kile walichodai hazifanyi kazi
ipasavyo na kuwasababishia usumbufu wa mara kwa mara na Polisi kutokana
na watendaji hao kutojadi kazi zao zaidi ya kujadi ushuru wanaokusanya.
Polisi
wa kutuliza ghasia wakijaribu Kuzuia Ghasia katika eneo hilo na
kufukuza Wamachinga kwa kuwatawanya kwa mabomu ya machozi.
Baadhi ya machinga na raia waliokuwa karibu na eneo la tukio wakitimua mbio kujihami na mabomu hayo.
Baadhi ya Machinga na raia wakiwa mbali na eneo la tukio baada ya kutimua mbio.
Watu mbalimbali wakitimua mbio ili kujiokoa na hatari katika eneo hilo. Picha zote na Latestnews Blog
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)