BOXING FEDERATION OF TANZANIA (BFT)
SLP 15558
DAR ES SALAAM
6/11/2011.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI;
YAH; KUSOGEZWA
MBELE KWA TAREHE YA KUFANYIKA KWA
KOZI YA WALIMU WA MCHEZO
WA NGUMI ZA RIDHA
SASA YATAFANYIKA TAREHE
17/11/2011 KIBAHA PWANI
Shirikisho la Ngumi
Tanzania (BFT) kwa kushirikiana na Kamati ya Olimpiki Tanzania(TOC)
wamelazimika kusogeza tarehe ya kufanyika kozi ya kimataifa ya walimu 30 wa
kufundisha mchezo wa ngumi.Sasa itafanyika kuanzia tarehe
17-25/11/2011 Kibaha
Pwani.
Awali kozi hiyo
ilikuwa ifanyike kuanzia kuanzia tarehe 12-18/11/2011 Kibaha Pwani.
Sababu ya kusogezwa
kwa kozi hiyo,imetokana na mkufunzi mkuu wa kozi hiyo,ambaye ameteuliwa na
Chama cha Ngumi cha Dunia (AIBA) Ndg Azzedin Aggoune kutoka Algeria,kuomba kozi
hiyo isogezwe mbele kutokana na yeye kupata dharula nchini kwao na kushindwa
kufika hapa nchini kama ilivyokuwa imepangwa.
Awali mkufunzi huyo ilikuwa
awasili hapa nchini tarehe 11/11/2011,kutokana na dharula iliyompata sasa
atawasili hapa nchini tarehe 16/11/2011.
Aidha kwa sasa
makocha hao watalazimika kuhudhuria mashindano ya Kova Cup yatakayoanza
kufanyika tarehe 14/11/2011 PR Stadium Hotel.zamani Imasco Centre.
Makore Mashaga
KATIBU MKUU BFT.
Mob;
0713588818.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)