Katibu
Mkuu wa Chadema, Dk Willbroad Slaa, akishuka kutoka kwenye Karandinga
la Polisi, kusomewa mashitaka yanayomkabili na washitakiwa wengine 26
waliofikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kwa kosa la kufanya
mkusanyiko kinyume na sheria.
--
KATIBU
Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa, Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu
Lissu pamoja na wanachama wengine 25 wa chama hicho wamekamatwa na
kupandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kwa tuhuma
za kufanya mkusanyiko usio halali.Mbali na hao, mwenyekiti wa chama
hicho, Freeman Mbowe ametakiwa kujisalimisha mwenyewe polisi baada ya
kutoweka katika Viwanja vya NMC Unga Limited baada ya polisi kufanya
operesheni ya kushtukiza kuwatawanya mamia ya wafuasi wa chama hicho na
viongozi wao waliokesha hapo usiku wa kuamkia jana.
Juzi, viongozi hao wa juu wa Chadema walitangaza kupiga kambi kwenye viwanja hivyo kwa siku tatu ikiwa ni shinikizo la kutaka mahakama itoe kibali maalumu cha kumtoa gerezani Kisongo, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema ambaye naye anatuhumiwa kufanya mkusanyiko usio halali.
Juzi, viongozi hao wa juu wa Chadema walitangaza kupiga kambi kwenye viwanja hivyo kwa siku tatu ikiwa ni shinikizo la kutaka mahakama itoe kibali maalumu cha kumtoa gerezani Kisongo, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema ambaye naye anatuhumiwa kufanya mkusanyiko usio halali.
Wengine
waliofikishwa mahakamani pamoja na Dk.Slaa kuhusu mashitaka hayo ni
Tundu Lissu,David Godfrey (18), Ally Hussein (20), Frank Chami (24),
Stella Mushi (21), Francis Smweli (20), Paulo Meena (18), Beatrice John
(28), Matei Thobias (38), Davies Sedeka (29) na Wilson Andrea (24).
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)