Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mh Lazaro Nyalandu Atembelea Wakala Wa Vipimo Na Mizani Jijini Dar es Salaam - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mh Lazaro Nyalandu Atembelea Wakala Wa Vipimo Na Mizani Jijini Dar es Salaam


Gari la kubeba mafuta kama lilivyokutwa likihakikiwa vipimo vyake katika karakana na Wakala wa Vipimo na Mizani.

 Meneja wa Vipimo Mkoa wa Ilala Bw Hamisi Hamidu (kushoto) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mh Lazaro Nyalandu ( Mwenye suti katikati) katika ziara yake Jijini Dar es salaam
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mh Lazaro Nyalandu( Aliechuchumaa kulia) na Meneja wa Vipimo na Mizani Mkoa wa Ilala Bw Hamisi Hamidu (kushoto) wakiangalia kipimo cha kutambua usahihi wa mafuta yanayopita katika pampu za kuuzia bidhaa hiyo.Wanaotazama ni maafisa wa Wakala wa Vipimo na Mizani na wenzao kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara.
  Aina mbali mbali za mizani zinazotumika katika kupima uzito wa bidhaa.
Picha ya pamoja ya wafanyakazi wa Wakala wa Vipimo na Mizani na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mh Lazaro Nyalandu(Aliekaa katikati) mara baada ya ziara yake kuwatembelea.
....
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mh Lazaro Nyalandu,jana ametembelea taasisi ya Wakala wa Vipimo na Mizani iliyo chini ya Wizara yake ili kuonana na wafanyakazi na kujionea baadhi ya shughuli zao.

Naibu Waziri Nyalandu amepokelewa na Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala huo Bwana Deo Maneno na kupewa taarifa ya utendaji wa taasisi hiyo ambayo imeonesha mafanikio makubwa katika kulinda haki za watumiaji hasa wakulima dhidi ya vipimo batili.

Akizungumza na Wafanyakazi na Vyombo vya habari mara baada ya ziara yake, Mh Nyalandu ameitaka taasisi hiyo kuongeza juhudi katika kudhibiti vipimo ili kuhakikiksha kuwa, watumiaji wanapata bidhaa na huduma zinazolingana na thanmani ya fedha wanazotoa.
Ameahidi kuusaidia Wakala huo ili kupata sheria mpya yenye nguvu zaidi kuliko ilivyo sasa ambapo wakosaji huamriwa kulipa faini ndogo zinazowafanya kuendelea kutumia vipimo batili bila wasiwasi wowote.

“ Kazi yenu ni muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa, watu wa kada zote wanawategemea katika kupata haki.. Kuanzia wakulima mpaka wanunuzi wa bidhaa za viwandani, wote wanataka vipimo sahihi,pigeni vita kangomba na lumbesa, shirikianeni na mamlaka nyingine kutimiza wajibu huu, wajengeeni watumishi wenu mazingira bora ya kazi, mtafanikiwa kuliko ilivyo sasa”, amesema Nyalandu

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages