Baadhi ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam
wakiingia katika eneo kunakotolewa huduma mbali mbali za upimaji wa
afya na matibabu katika mabanda ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii
yaliyopo katika viwanja vya Mnazi Mmoja ikiwa ni katika maadhimisho ya
miaka 50 ya Uhuru katika utoaji huduma za afya Tanzania.
Afisa Muuguzi Sista Zania Ndimbo kutoka
Hospitali ya Amana akitoa huduma kwa mmoja wa watu waliojitokeza kupima
ugonjwa wa Kisukari.
Muuguzi Asma Msimbe akichukua vipimo vya
damu kwa ajili ya kupima Ugonjwa wa Kisukari kwa mmoja watu
waliojitokeza kupima Afya zao
Baadhi ya wananchi wakisubiri
katika foleni ya kupata huduma ya Bure ya uchunguzi na matibabu ya
Saratani ya Matiti kwa kina Mama.
Baadhi ya wananchi wakiwa katika foleni
katika banda linalotoa huduma ya Upimaji na Mtibabu ya Macho bure.
Moja wapo ya bango lililopo katika eneo la
kuingilia katika mabanda yanayotoa huduma hizo likionyesha huduma
zinazotolewa bure kwa watu wote kwa kipindi chote cha maadhimisho hayo.
Afisa Muuguzi Sista Zania Ndimbo kutoka
Hospitali ya Amana akitoa huduma kwa mmoja wa watu waliojitokeza kupima
ugonjwa wa Kisukari.
Katika Banda la Ushauri Nasaha na Upimaji
VVU lililopo katika viwanja vya Mnazi Mmoja Muuguzi Mshauri Rehema
Kessy akitoa maelekezo sahihi ya jinsi ya kutumia mipira ya kiume
Kondom kwa kijana Frank Christopher.
Bendi ya Mjomba ikitoa burudani katika
viwanja vya Mnazi Mmoja ambapo wananchi wanapata Ujumbe kupitia muziki
huo na burudani pia huku Upimaji wa Afya zao bure ukiendelea.





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)