WATANZANIA WAOMBWA KUIPIGIA KURA NEMBO YA HAKI ZA BINADAMU. - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

WATANZANIA WAOMBWA KUIPIGIA KURA NEMBO YA HAKI ZA BINADAMU.

Katibu mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bi. Mary Massay akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu zoezi la upigaji wa kura linaloendelea duniani kote kwa ajili ya kupata Nembo rasmi ya Haki za binadamu itakayotumika duniani, Tanzania ikiwa miongoni mwa nchi zilizoridhia mkataba wa wa kimataifa wa Haki za Binadamu inashiriki zoezi hilo kwa wananchi kupiga kura kuchagua nembo inayofaa kati ya kumi zilizopendekezwa kupitia mtandao wa www.humanrightslogo.net kabla ya tarehe 17 mwezi huu.
Katibu mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bi. Mary Massay (katikati) akiwa na balozi wa Canada nchini Tanzania Robert Orr (kushoto) na Mshauri msaidizi anayeshughulikia zoezi la uhamasishaji wa kupiga kura kutoka ubalozi wa Ujerumani Bw. Hans Koeppel (kulia) kwa pamoja wakionyesha nembo kumi ambazo zinapigiwa kura na mataifa mbalimbali kupitia mtandao wa www.humanrightslogo.net ambapo nembo itakayopata kura nyingi itawasilishwa tarehe 23 mwezi huu kwenye mkutano wa Umoja.
Katibu mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bi. Mary Massay (katikati) akijadili jambo na balozi wa Canada nchini Tanzania Bw. Robert Orr (kushoto) na Mshauri msaidizi anayeshughulikia zoezi la uhamasishaji wa kupiga kura kutoka ubalozi wa Ujerumani Bw. Hans Koeppel (kulia) leo jijini Dar es salaam wakati wa mkutano wa uhamasishaji wa watanzania kushiriki zoezi la kupiga kura ya Nembo ya Haki za binadamu.
Balozi wa Canada nchini Tanzania Robert Orr akizungumza na waandishi wa habari na wajumbe mbalimbali waliohudhuria mkutano wa uhamasishaji wa Tanzania (watanzania) kushiriki zoezi la kupiga kura kwa ajili ya kupata nembo rasmi itakayotumika kimataifa kwa ajili ya shughuli za Haki za Binadamu leo jijini Dar es salaam. Pamoja na mambo mengine balozi huyo amesema watanzania wanaomchango mkubwa katika kupiga kura ili ipatikane nembo moja kati ya kumi zilizopendekezwa na washindi wa tuzo za Amani na wanaharakati mashuhuri wa Haki za Binadamu duniani.Picha na Aron Msigwa – MAELEZO.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages