WASHIRIKI WA SHINDANO LA GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE WAANZA KUZISAKA DOLA 50.000 KILA WIKI - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

WASHIRIKI WA SHINDANO LA GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE WAANZA KUZISAKA DOLA 50.000 KILA WIKI

Wapenzi wa kinywaji mahiri cha Guinness na mashabiki wakubwa wa mpira wa miguu nchini Tanzania, kwa mara ya kwanza leo wamekusanyika katika viwanja vya Leaders kwa ajili ya kushiriki katika GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ ambayo imezinduliwa leo katika viwanja hivyo.
Washiriki wengi wamejitokeza ili kujisajiri na kuonyesha maajabu ya mpira wa miguu katika kipindi hiki kabambe cha Televisheni ambacho kinaangaliwa na kuwavutia watu wengi barani Afrika,Shindano hili litawapatia mashabiki nchini Tanzania nafasi ya kujitokeza na kuonyesha mapenzi yao ya dhati katika mpira wa miguu na kushindana na mashabiki wakubwa wa mpira wa miguu kutoka Kenya na Uganda huku kujishindia mamilioni ya fedha.
Katika picha juu kushoto ni Meneja wa kinywaji cha Guinness Moris Njowoka akumuelekeza jambo Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Serengeti Breweriers Ephraim Mafuru wakati wa shindano hilo leo.
Baada ya kupatika na timu nane zitakazokuwa na watu wawiliwawili , timu hizo zikishiriki katika shindano hilo kupitia Luninga (Television) likirushwa mara moja kila wiki Televisheni kwa muda wa wiki nane, na kila wiki atapatikana mshindi mmoja atakayejishindia Dolla za Kimarekani 50.000,
Shafii Dauda Mtangazaji wa Clouds FM akiwaelekeza jambo washiriki wa shindano la Guinness Football Challenger katika viwanja vya Leaders leo.
Mmoja wa washiriki katika shindano hilo akionyesha uwezo wake katika kumiliki mpira wa miguu kama anavyoonekana.
Mshiriki huyu naye alionyesha uwezo mkubwa katika kumiliki mpira kwa kupiga danadana kana wanavoonekana washiriki wenzake wakimuangalia.
Washiriki wa shindano la Guinness Football Challenge wakipata maelezo mbalimbali kutoka kwa waratibu wa shindano hilo.Habari Kwa Hisani Ya Full Shangwe Blogu

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages