MASHINDANO YA MASHUA YA JOHNNIE WALKER THE LASER OPEN COMPETITION YAMALIZIKA LEO JIJINI DAR ES SALAAM - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

MASHINDANO YA MASHUA YA JOHNNIE WALKER THE LASER OPEN COMPETITION YAMALIZIKA LEO JIJINI DAR ES SALAAM

Mwendesha mashua bora wa Afrika Mashariki Al Bush akipokea kikombe chake cha ushindi kutoka kwa Benjamin Mariki Meneja wa vinywaji vikali kutoka kampuni ya Serengeti Breweriers (SBL), mara baada ya kuwashinda waendesha mashua wenzake kutoka nchi 15 katika mashindano ya Johnnie Walker THE LASER OPEN COMPETITION yaliyoanza juzi na kumalizika leo kwenye klabu ya Dar es salaam Yacht Club (DYC) Masaki jijini Dar es salaam. Mwendeshaji huyo wa mashua Bw. Al Bush amesema amekuwa akiendesha mashua kwa muda wa miaka 25 sasa na amekuwa mshindi katika mashindano hayo kwa miaka 9 katika mashindano yaliyofanyika nchi mbalimbali za Afrika Mashariki. Katika picha kulia ni anayeshuhudia ni Hellen Rattansi Meneja Mauzi na Masoko. Kampuni ya bia ya Serengeti Breweriers SBL ndiyo iliyodhamini mashindano kupitia vinvywaji vyake vikali vya John Walker na yaliomalizika leo jijini Dar es salaam
Bw Richard Hamer akipozi kwa picha mara baada ya kupokea zawadi yake ya chupa ya kinywaji (WINE) kutoka kwa Tom Vanneste katikati mratibu wa mashindano hayo, kushoto ni Hellen Rattansi Meneja Mauzi na Masoko.
Hellen Rattansi Meneja Mauzo na Masoko akimkabidhi Ype Smit zawadi yake ya kinywaji cha Wine mara baada ya kufanya vizuri katika mashindano ya Johnnie Walker THE LASER OPEN COMPETITION yaliyomalizika leo jijini Dar es salaam
Meneja Masoko wa Serengeti Breweriers Emilian Rwejuna kulia akikabidhi zawadi Mwambao Jumbe Mmjoa wa washiriki wa mashindano ya kuendesha mashua Johnnie Walker THE LASER OPEN COMPETITION.
Kutoka kulia ni Hellen Rattansi Meneja Masoko na Mauzo, Benjamini Mariki Meneja wa Vinywaji vikali vya John Walker, Emilian Rwejuna Meneja Masoko (SBL) na Mark Hart Real Comodole Sail (DYC).
Washiriki mbalimbali wakiangalia wakati wa utoaji wa zawadi kwa washindi wa mashindano hayo.
Kutoka kulia ni Meneja Masoko wa Serengeti Breweriers (SBL) Emilian Rwejuna , Benjamin Mariki Meneja wa Vinywaji vikali vya Johnnie Walker na Tom Vanneste Mratibu wa Mashindano hayo wakijadiliana jambo wakati wa utoaji zawadi kwa washindi wa shindano hilo.
Washiriki wa mashindano ya Johnnie Walker THE LASER OPEN COMPETITION wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa mashindano hayo na kupokea zawadi kwa washindi.
Kikundi cha Burudani kikitumbuiza katika hafla ya utoaji wa zawadi kwa washindi wa Johnnie Walker THE LASER OPEN COMPETITION.
Meneja Masoko wa Serengeti Breweriers (SBL) Emilian Rwejuna akizungumza na washiriki wa mashindano hayo wakati wa hafla ya utoaji zawadi kwa washindi.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages