Washiriki wa shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, wakipiga picha na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya simu ya Vodacom
NA LYSBERT MORAGWA, SAUT
WAREMBO
wanaowania taji la Vodacom Miss Tanzania 2011, kesho wanatarajia
kuchuana katika kuonyesha vipaji vyao katika michezo, kwenye ufukwe wa
Jangwani Sea Breeze, Dar es Salaam.
Tukio
hilo litakaloanza saa 3:00, ni miongoni mwa vipengele (fast tracks)
vitano vya awali vya kinyang’anyiro hicho ambapo washindi hutinga moja
kwa moja katika hatua ya nusu fainali.
Tayari
warembo wawili wameshapata tiketi ya kuingia nusu fainali ya
mashindano hayo ambao ni Mwajabu Juma aliyeshinda taji la Top Model na
Tracy Sospeter aliyeshinda taji la Miss Photogenic.
Mbali
ya vipengele hivyo, vingine vilivyobaki ni Kipaji (Talent) na Mvuto
(Personality) ambapo mshindi wake hutangazwa kila wiki kabla ya fainali
za taifa zilizopangwa kufanayika Septemba 10, mwaka huu katika Ukumbi
wa Mlimani City, jijini.
Kwa
mujibu wa Mkurugenzi wa Lino International Agency, waandaaji wa
shindano hilo, Hashim Lundenga, michezo itakayohusishwa leo ni riadha,
mbio za magunia, kuogelea, kuruka chini, mpira wa miguu, mpira wa pete,
kuvuta kamba na mingineyo.
Shindano
la Vodacom Miss Tanzania 2011, limedhaminiwa na Vodacom, Redd’s
Original, New Habari (2006) Ltd, Star TV, Giraffe Hotel na Papa Zee
Entertainment.





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)