MUFTI WA TANZANIA SHEIKH MKUU, ISSA SHAABAN BIN SIMBA AKABIDHIWA MILIONI 13 NA EDWARD LOWASSA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

MUFTI WA TANZANIA SHEIKH MKUU, ISSA SHAABAN BIN SIMBA AKABIDHIWA MILIONI 13 NA EDWARD LOWASSA


Waziri Mkuu wa zamani,Edward Lowassa(Kushot0)akimkabidhi Bahasha yenye Tsh. milioni 13, Mufti wa Tanzania, Sheikh Mkuu,Issa Shaaban bin Simba,kwa ajili ya kusaidia shule ya sekondari la Edward Lowassa iliyopo Kigamboni,Dar es Salaam.Kwa mujibu wa Mufti ambaye ni mlezi wa shule hiyo, Shule hiyo inatarajiwa kufunguliwa rasmi mwakani kwa kuanzia na wanafunzi 200 wa kidato cha kwanza, na kwamba fedha hizo zitatumika kukamilisha baadhi ya mambo ya shule hiyo ikiwemo kujenga bweni la watoto 30, choo cha shule, kisima cha maji na shule itajihusisha zaidi kusomesha yatima na watoto wanaoishi katika mazingira magumu. Kulia ni aliyekuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Alfred Tibaigana ambaye pia ni mlezi wa shule hiyo.
Edward Lowassa(kulia)akimsindikiza Mufti wakati akiondoka baada ya hafla ya kumkabidhi fedha hizo,iliyofanyika Ofisini kwake,Mikocheni, Dar es Salaam.
Wakiagana  baada ya shughuli hiyo.Picha na Mdau Bashir Nkromo

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages