IGP Said Mwema Azindua Kampeni Ya Uvaaji Wa Helmet na Usalimishaji wa Silaha Nchini - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

IGP Said Mwema Azindua Kampeni Ya Uvaaji Wa Helmet na Usalimishaji wa Silaha Nchini


IGP Mwema akijibu maswali mbalimbali wakati wa uzinduzi wa kuanza kuhakiki silaha nchini, uvaaji helmeti na uhamasishaji jamii kutii sheria bila kusurutishwa
Kamishna wa Polisi, Clodwin Mtweve akisisitiza jambo katika mkutano huo
Mkuu wa Oparesheni wa Jeshi la Polisi, Kamishna Paul Chagonja akifafanua mbamo mbalimbali hasa kuhusu oparesheni iliyotangazwa jana  na IGP, Mwema ya kusalimisha silaha zinazomilikiwa isivyo halali
Mkuu wa kitengo cha Polisi cha Maboresho, Lucas Kusima akielezea kuhusu maboresho mbalimbali yaliyofanywa na jeshi hilo
Mkuu wa kitengo cha upelelezi wa makosa mtandao,Kasala,akielezea jinsi wanavyopambana na uhalifu huo
IGP Mwema akikata utepe kuashiria uzinduzi huo
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP, Said Mwema (katikati) akivishwa helmeti baada ya Taasisi ya Helmet Vaccin Initiative Tanzania, kukabidhi msaada wa helmeti 500 kwa jeshi hilo, wakati wa hafla ya uzinduzi wa uhamasishaji jamii kuvaa kofia hizo wakipanda pikipiki, Dar es Salaam jana katika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP, Said Mwema (katikati) akiangalia wakati Balozi wa Hiari wa Uvaaji wa Kofia nchini, Ritta Poulsen (kulia kwake) baada ya Taasisi ya Helmet Vaccin Initiative Tanzania, ilipokabidhi msaada wa helmeti 500 kwa jeshi hilo, wakati wa hafla ya uzinduzi wa uhamasishaji jamii kuvaa kofia hizo wakipanda pikipiki Dar es Salaam jana.Picha Zote na Mdau  Richard Mwaikenda

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages