Serikali
imepanga kufanya sensa ya watumishi wote wa serikali na taasisi zake
kwa kuandaa siku maalum ya kuwalipa wafanyakazi wote dirishani ili
kuthibiti mishahara hewa.
Akiwasilisha
hotuba ya bajeti ya mwaka wa fedha 2011/2012, Waziri wa Fedha na Uchumi
Mustapha Mkullo amesema Wakuu wa Idara watawajibika kwa kuhakikisha
kwamba wafanya kazi wanaolipwa ni halali.
MKULLO
amesema kwamba watendaji wote wa Halmashauri na taasisi za serikali
watawajibika ikibainika kwamba serikali imelipa mshahara kwa
wafanyakazi hewa.
Na East Africa Blog.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)