KESI YA MPENDAZOE YATUPILIWA MBALI - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

KESI YA MPENDAZOE YATUPILIWA MBALI



Bw Fred Mpendazoe 
-----
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imetoa amri ya kuondolewa kwa hati ya madai ya kesi ya kupinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 wa Jimbo la Segerea iliyokuwa imefunguliwa na aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya (CHADEMA), Fred Mpendazoe dhidi ya mbunge wa sasa (CCM), Dk.Makongoro Mahanga na wenzake mahakamani hapo baada ya kubaini hati hiyo ina mapungufu yanayosababisha wadaiwa kushindwa kuaandaa utetezi wao.

Mbali na Mahanga ambaye ni Naibu Waziri wa Kazi na Ajira wengine ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Segerea ambapo mdaiwa wa kwanza na wa pili wanatetewa na mawakili wa serikali David Kakwaya na Patience Ntwina na Mahanga anatetewa na wakili wa kujitegemea Jerome Msemwa.

Uamuzi huo ulitolewa jana mchana na Jaji Profesa Ibrahim Juma ambapo alisema kesi hiyo jana ilikuja kwaajili ya yeye kutolea uamuzi mapingamizi matatu yaliyowasilishwa mbele yake na upande wa utetezi Mei 25 mwaka huu, ambayo yaliomba mahakama hii itoe amri ya ama ya kuifuta kesi hii au kuamuru hati ya madai ifanyiwe marekebisho kwasababu baadhi ya aya zilizopo ndani ya hati hiyo zina mapungufu yanayonyima haki wadaiwa kuandaa utetezi wao.
Kwa Habari zaidi  <<<< BOFYA HAPA >>>>

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages