WAZIRI WA AFYA AZINDUA KAMPENI YA KITAIFA YA KUPUNGUZA VIFO VYA WANAWAKE WAJAWAZITO NA WATOTO CHINI YA MIAKA 5 JANA JIJINI DAR ES SALAAM - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

WAZIRI WA AFYA AZINDUA KAMPENI YA KITAIFA YA KUPUNGUZA VIFO VYA WANAWAKE WAJAWAZITO NA WATOTO CHINI YA MIAKA 5 JANA JIJINI DAR ES SALAAM


Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dr Haji Mponda akisoma hotuba ya ufunguzi rasmi wa kampeni ya Kitaifa ya kuzuiavifo vya akina mama na watoto chini ya umri wa miaka mitano leo mchana katika viwanja vya Mnazimmoja jijini Dar es Salaam. Dr Mponda alisema kuwa asilimia 25 ya akina mama wajawazito wanaokufa kutokana na uzazi vifo vyao hutokana na kuvuja damu nyingi wakati wa kujifungua au baada ya kujifungua. Pia alisema kuwa watoto wengi wanaokufa chini ya umri wa miaka mitano asilimia 22 ya vifo hivyo hutokana na kuugua ugonjwa wa malaria ambapo sababu ya vifo ni upungufu wa damu. Dr Mponda alisema kuwa Serikali imeweka mikakati madhubuti kuhakikisha kuwa vituo vya afya na vinakuwa na wataalamu wa kutosha. Zahanati kujengwa katika kila kijiji na Vituo vya afya katika kila kata ili kusogeza huduma za afya karibu na wananchi.
Msanii wa mashairi Mrisho Mpoto akiwa na wanafunzi mbele ya meza ya mgeni rasmi wakati akitoa burudani leo mchana katika viwanja vya mnazi mmoja katika Uzinduzi wa kampeni ya kupunguza vifo vya akina mama na watoto chini ya miaka mitano
Waziri wa afya Dr Haji Mponda akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi  wa kampeni ya kitaifa ya kupunguza vifo vya wanawake na watoto,  Kushoto ni waziri wa Wanawake, Jinsia na Watoto Sophia Simba.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Haji Mponda akiwa amepanda katika moja ya piki[iki maalumu kwa ajili ya kubebea wagonjwa hususani maeneo ya vijijini. Dr Mponda alisema kuwa  serikali imejipanga kusambaza pikipiki 421 nchini kote  na tayari pikipiki 51 zimekwisha sambazwa katika mikoa ya Pwani, Morogoro na Shinyanga.
. Dr Mponda akionesha kifurushi maalumu chenye vifaa muhimu vya kuzalishia.Vifurushi hivyo vitaanzan kusambazwa bure kwa akina mama wajawazito nchini kote ili kuwaepushia adha ya kununua vifaa hivyo pindi wanapokaribia kujifungua
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dr Haji Mponda akipata maelekezo toka kwa muelimishaji rika katika moja ya mabanda yaliyokuwa yakitoa huduma katika viwanja vya mnazi mmoja leo mchana.
Moja ya msanii wa kikundi cha sanaa cha Bagamoyo akiwa anaigiza igizo lililokuwa na maudhui ya madhara ya uchache wa wahudum wa afya katika vituo vya kutolea tiba hali inayopelekea akina mama wengi  wajawazito kufa kwa kukosa huduma kwa wakati.  Picha zote na Mdau  Victor Makinda

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages