JUST IN: UDOM WAWAZIDI MAARIFA ASKARI KWA KUINGIA MJINI BILA ASKARI KUTAMBUA, KUJA KUSHTUKA WANAFUNZI WAKUSANYIKA VIWANJA VYA MWALIMU NYERERE SQUARE ASUBUHI YA LEO - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

JUST IN: UDOM WAWAZIDI MAARIFA ASKARI KWA KUINGIA MJINI BILA ASKARI KUTAMBUA, KUJA KUSHTUKA WANAFUNZI WAKUSANYIKA VIWANJA VYA MWALIMU NYERERE SQUARE ASUBUHI YA LEO

Wanafunzi Wa Udom Kutoka Vitivo Viwili Cha Sayansi Ya Jamii, Sanaa na Lugha Pamoja Na Kitivo Cha Sayansi Asilia Wakiwa Wamekutana Katika Viwanja Vya Nyerere Square Baada Ya Kuwazidi Maarifa Polisi Waliojitahidi Kuwazuia Barabarani Wakati Wanafunzi Walipita Njia Za Mikato Hadi Kufika Viwanjani hapo
Mwanafunzi Wa UDOM akiwa amebeba Bango ambalo Linasema "Pinda Adanganya Tena Must Step Down" Mara Baada Ya Kukutana Katika Viwanja Vya Nyerere Square.
Mwanafunzi Akiwa Amebeba Bango linalosema 
 "Bila Field (Mafunzo Kwa Vitendo) UDOM ni Shule ya Sekondari" Wakati wamekusanyika Katika Viwanja Vya Nyerere Square Asubuhi Hii
 Wanafunzi Wa Vitivo Viwili Kutoka Chuo KIkuu Cha Dodoma Wakiwa Wamekusanyika Katika Uwanja Wa Nyerere Square Asubuhi ya Leo Mara baada ya kuwazidi akili polisi ambao walijipanga kuwazuia wanafunzi hao barabaranii wakati wanafunzi wakatumia njia za mikato na hatimaye kufika viwanjani hapo
 Wanafunzi Wakimsikiliza Raisi Wa Kitivo Cha Sayansi Ya Jamii Mh Mwakinbinga Wakati Akitoa Maelekezo Jinsi Ya Kuweza kufika Bungeni Kuonana Na Waziri Mkuu Na Waziri Wa Elimu
 Raisi Wa Kitivo Cha Sayansi Ya Jamii, Sanaa na Lugha Akitoa Maelekezo Juu Ya Kufika Bungeni KUonana na Waziri Mkuu
 Waandishi Wa Habari kutoka Vyombo Mbalimbali Vya Habari Wakichukua Habari Wakati Raisi Wa Vitivo hivyo Viwili Wakitoa Maelekezo Muhimu
 Wanafunzi Walipokua Wakiimba Nyimbo za Ukombozi Pamoja Na Wimbo Wa Taifa Na Tanzania Tanzania
 Maraisi Wa Vitivo Mh Mwakibinga Wa Sayansi Ya Jamii, Sanaa na Lugha( Wa Kulia) Na Lema Wa Kitivo Cha Sayansi Asilia Wakiteta Jambo Mara baada Ya kutoa Maelekezo Kwa Wanafunzi Waliokusanyika Viwanjani hapo
Wanafunzi Wa UDOM wakijiandaa kuelekea Bungeni Wakitokea Viwanja Vya Nyerere Square Asubuhi hii

 Vijana Wa IGP Mwema Wakiwa Tayari Nje ya Uzio Wa Nyerere Square Kwaajili Ya Kuwazuia Wanafunzi Wasifike Maeneo Ya Bunge Lakini Bado Waliweza Kukubali Kushindwa na Kuzidiwa Maarifa Na Wanazuoni Hao Kwa Kuzidiwa Maarifa na HAtimaye wanafunzi kuweza Kupita na kukaribia maeneo ya bunge na hapo ndio mabomu yalipoanzaa kusikika
 Askari Polisi Wakiwa Wamejiandaa Kwa ajili Ya kuwazuia Wanafunzi Hao Lakini Walionyesha kushindwa kete na wanafunzi kukaribia maeneo ya bunge huku wengi wakiwa wamefika na Hatimaye mabomu kulindima Maeneo ya Bunge
Kaa Tayari kama Wanavyoonekana hapo wakiwa na shauku ya kupiga

Hatimaye Polisi Wameweza Kukubali kushindwa na Kuzidiwa Kete wakati wa kuwazuia Wanafunzi Wasiweze kufika Mjini Dodoma Kwaajili Ya Kuelekea Bungeni Kuonana Na Waziri Mkuu Mh Pinda Kwaajili ya kutoa Malalamiko yao kuhusu kufutwa Kwa Mafunzo Kwa Vitendo (FIELD) kama Walivyokubaliana Mwanzo

Hapo Awali wanafunzi Wa Kitivo Cha Sayansi Asilia Waliweza Kuwahi Kuamka Na kuelekea Mjini Na Kufanikiwa Kufika Karibu Na Mjini Lakini Polisi Hao Waliweza Kuwazuia Kwa Muda Lakini Bila Mafanikio Wanafunzi Waliweza Kugawanyika Makundi na Kupita Njia Tofautitofauti Na Kukutana Katika Viwanja Vya Mwalimu Nyerere Square kwaajili ya kujipanga upya

Polisi Kwa Kujua Kuwa Waliowazuia Mwanzo Ndo Chuo Kizima Na Kusahau Au Bila Kujua Kuwa Kuna Kitivo Kingine Kinakuja waliweza kuchanganyikiwa ni wapi pa kuwazuia wanafunzi wa kitivo cha sayansi ya jamii, sanaa na lugha Ambao Walionyesha umahiri wa hali ya juu wa kuweza kupita njia za mikato hadi kufika mjini pamoja na polisi wachache kuweza kujua walipopita lakini walishindwa kufika na kupiga bomu moja la machozi ambalo halikumwasiri mtu yeyote yule

Baada ya Wanafunzi Hao Wa Vitivo Vyote Viwili Kufanikiwa Kufika Viwanja Vya Nyerere Square Na Kupanga Mikakati kabambe ya Kuelekea Bungeni Wanafunzi Hao Walianza Kuondoka Na Kuelekea Bungeni Huku Polisi Wakiwa hawajui cha kufanya kwa kuzidiwa ujanja HAtiamye polisi Waliweza kuwazuia Wanafunzi Hao Katika Makutano ya Barabara Ya Standi Kwa Kuwalushia Mabomu ya Machozi Wakati wanafunzi wanakimbilia sehemu mbalimbali wanafunzi hao waliweza kukutana tena maeneo ya sokoni ambapo askari waliweza kuwafuata na kupiga mabomu ya machozi ambayo wanafunzi walionyesha kuwa walijiandaa na kuanza kunawa kwa maji waliyobeba wakati wakitoka chuo.

Wakati wanafunzi hao Wakiwa Wametawanyika sehemu mbalimbali za Mji Wa dodoma Wanafunzi waliweza kuharibu bidhaa za watu ambao walikua sokini wakati wa kukimbia kwaajili ya kunusuru Maisha yao.
 Baada ya Dakika Si Zaidi Ya Kumi na Tano Wanafunzi Hao waliweza kukutana Tena Viwanja Vya Nyerere Square Na Ndipo Mkuu Wa Mkoa Dr Msekela Kufika Na Kuwaambia Wanafunzi Kuwa Wasubiri Waziri Wa Elimu Mh Kawambwa Anakuja Kuongea Na wanafunzi Hao.

Muda Zaidi Ya Saa Moja Na Nusu Waziri Wa Elimu Hakutokea Na Hatimaye Wanafunzi Wakaanza Tena Kuimba Nyimbo za Ukombozi Na Hatimaye polisi Wakafika Tena Viwanjani hapo Na kuwatawanya Wanafunzi hao.
Mpaka Naingia Mitambo Wanafunzi Waliokamatwa wanafikia 30 huku wengine wakiachiwa na Mpaka Sasa waliopata majeraha wanakadiriwa kufikia 7 ambapo inasemekana mmoja wa majeraha Hao Amevunjika Mguu Mara baada ya kupigwa na polisi na Hatimaye kumtelekeza hapo na ndio wananchi wenye moyo safi kumchukua na Kumpeleka Hospitali ya Mkoa Wa Dodoma kwaajili ya matibabu
Mpaka Muda huu Inasemekana Waziri Wa Elimu Mh Kawambwa na Mkuu Wa Mkoa Dr Msekela wamefika Ofisi Za Chuo Kuongea na Viongozi Wa Juu Wa Chuo.
Lakini Hali inavyoonekana Hadi muda huu ni kuwa Mgomo Bado unaendelea japokuwa kuna tetesi kuwa wanafunzi hao wameambiwa warudi chuo kwaajili ya kusubiri Waziri Wa ELimu Aje kuongea Nao Saa Kumi Lakini Wanafunzi Hao Wanesema Kuwa Asipokuja na Maelezo ya Kuwa ni Lini Wataenda kufanya mafunzo Kwa Vitendo na Lini Pesa yao Itaingia kabla ya kufanya Mitihani yao ya kumaliza Muhula ambayo inaanza tarehe 20 june 2011 Basi Mgomo utaendelea na ambapo kama wataendelea na mgomo huo hapo kesho watakuwa wamebakiza siku moja ili chuo kifungwe kutoka na katiba ya TCU na Bunge Kuwa Chuo Wakigoma Siku Tatu Mfululizo Basi Chuo Kifungwe.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages