Mchezaji
wa timu ya Simba Mussa Hassan Mgosi akiwa amembeba mchezaji mwenzake
Amri Kiemba mara baada ya kupachika goli la kwanza na la ushindi,
katika goli la timu ya Motema Pembe kutoka DRC kwenye mchezo wa michuano
ya Kombe la Shirikisho la CAF, uliochezwa katika uwanja wa Taifa
jijini Dar es salaam jioni hii, goli hilo limefungwa kipindi cha kwanza
dakika ya 20 ya mchezo huo mshabuliaji Mgosi aliipokea pasi nzuri kutoka
kwa kiungo Mohamed Banka kufunga goli hilo pekee, hivyo Simba
imefanikiwa kuwatoa "ulimi nje" wapinzani wao Motema Pembe ya DRC.
Mchezaji
Emmanuel Okwi akimtoka beki wa timu ya Motema Pembe katika mchezo wa
Kombe la Shirikisho la CAF katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Mshika
kibendera akiangalia wakati wachezaji wa timu ya Simba na Motema Pembe
wakichuana katika mchezo wao unaofanyika sasa kwenye uwanja wa Taifa
Credits: Full Shangwe Blogu
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)