YUPI NI MKWELI KATI YA OBAMA NA OSAMA..NA LIPI LA UKWELI KUHUSU KIFO CHA OSAMA. - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

YUPI NI MKWELI KATI YA OBAMA NA OSAMA..NA LIPI LA UKWELI KUHUSU KIFO CHA OSAMA.

 
Sifael Paul na Mashirika ya Kimataifa
Nyuma ya taarifa ya kifo cha kiongozi wa kundi la kigaidi duniani la Al-Qaeda, Osama bin Mohammed bin Awad bin Laden (54), kuna utata mtupu ikielezwa kwamba inawezekana jamaa huyo akawa hajafa, Risasi Mchanganyiko linashuka nayo hatua kwa hatua.

Taarifa iliyotolewa usiku wa kuamkia Jumatatu ya Mei 2, 2011 na kuthibitishwa na Rais wa Marekani, Barack Hussein Obama ilisema kuwa, Osama aliyezaliwa Machi 10, 1957 aliuawa na vikosi vya ulinzi vya nchi hiyo katika eneo la Abbottabad nchini Pakistan alikokuwa amejificha.
Kwa mujibu wa mtandao mmoja nchini Pakistan muda mfupi baada ya kutolewa taarifa hiyo, tukio hilo lilikosa ushahidi wa kutosha kuuthibitishia ulimwengu namna kiongozi huyo alivyouawa.

“Tunachojua Osama ni mzima. Haitoshi kusema ameuawa bila ushahidi wowote na isitoshe picha iliyotolewa ni ile ya Osama ya miaka kumi iliyopita.

“Ameuawa vipi? Ina maana sisi wote tunaamini kile wanachokisema Wamarekani bila uthibitisho? Hata kama ni hivyo, watu hawawezi kuamini kuwa alishakufa siku nyingi kwa ugonjwa?

“Tunachojua alikuwa mgonjwa tangu alipohusishwa na mashambulizi ya Septemba 11, 2001,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.
Kwa Habari Zaidi  <<< BOFYA HAPA >>>

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages