OBAMA ALISHUHUDIA LIVE KIFO CHA OSAMA BIN LADEN - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

OBAMA ALISHUHUDIA LIVE KIFO CHA OSAMA BIN LADEN



Exuper Kachenje, Andrew Msechu na Mashirika
RAIS Barrack Obama wa Marekani alishuhudia moja kwa moja (live) jinsi makomandoo 100 wa jeshi lake wakitekeleza shambulizi na hatimaye ‘mazishi’ ya kiongozi wa mtandao wa kigaidi wa al Qaeda, Osama Bin Laden.
Operesheni hiyo ilishuhudiwa pia na Makamu wa Rais Joe Biden, Waziri wa Mambo ya Nje, Hillary Clinton, Mkurugenzi wa Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA), Leon Panetta na viongozi wengine wa ngazi ya juu. Makomandoo hao walifanya kazi hiyo usiku wa giza nene wakiwa wamevaa miwani maalumu iliyowawezesha kuona.
Ilikuwa kama sinema wakati walipokuwa wakiendesha operesheni hiyo. Obama aliangalia tukio hilo zima akiwa Ikulu ya Marekani ya Washington-DC. Kazi hiyo ilitumia dakika 40 na kuhitimisha miaka 10 ya kujificha na kuwa tishio la mashambulizi ya kigaidi.
Kushuhudiwa huko moja kwa moja kwa operesheni hiyo, kuliwezeshwa na makomandoo hao kwani walivaa kamera maalumu zilizorekodi matukio yote yaliyokuwa yakifanyika na kuyarusha moja kwa moja hadi Ikulu ya Marekani na Makao Makuu ya CIA.
Kwa Habari Zaidi  <<< BOFYA HAPA >>>

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages