Katika mashindano ya wanaume, Martin Lel alichukua nafasi ya pili, huku mwenzake kutoka Kenya, Patrick Makau, akimaliza katika nafasi ya tatu.
Wakenya walitwaa ubingwa kwa kuchukua nafasi zote tatu za kwanza katika mashindano hayo.
Bingwa mtetezi katika mashindano ya wanawake, Liliya Shobukhova kutoka Urusi, alichukua nafasi ya pili.
Shobukhova alionekana kushabikiwa sana kuwa atashikilia ubingwa wake wa London Marathon na alikuwa akiongoza mwanzoni mwa mashindano hayo, lakini Keitany aliongeza kasi alipofika maili 15 na kuendelea hivyo hadi tamati.
Edna Kiplagat mwenye umri wa miaka 31 alichukua nafasi ya tatu na hii ni mara yake ya kwanza kushiriki katika mashindano haya ya riadha ya London Marathon.
Keitany alianza riadha mwaka 2007 kama mchochea kasi na aliibuka mwanamke wa 10 kukimbia kwa muda wa saa mbili na dakika 20.
Mwanariadha huyo sasa ana nafasi nzuri ya kushiriki katika Olympic Marathon mwaka 2012.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)