‘MASANJA’, WALOKOLE WENZAKE WANUNUA SHANGA, VIDANI MORO - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

‘MASANJA’, WALOKOLE WENZAKE WANUNUA SHANGA, VIDANI MORO

Masanja (wa pili kulia ngazi ya pili) akiwa na wanakwaya wenzake wakinunua shanga na vidani.
NA DUNSTAN SHEKIDELE, MOROGORO
MSANII nyota wa kundi la vichekesho la shirika la utangazaji la TBC1 liitwalo Orijino Komedi, Emmanuel Mgaya 'Masanja Mkandamizaji', Jumatatu Pasaka ya Pili alinaswa na matandao huu akinunua shanga na vidani kwenye tamasha la uzinduzi wa  albam ya video ya kwaya ya Agape uliofanyika ndani ya uwanja wa soka wa  Jamhuri mkoani Morogoro.

Mbali na kuigiza, Masanja ni mlokole anayesali katika kanisa la kilokole la EATG Mito ya Baraka la jijini Dar es Salaam ambapo msanii huyo ni miongoni mwa wanakwaya wa kanisa hilo inayojulikana kwa jina la Jerusalem.

Kwaya hiyoni miongoni mwa zilizoalikwa katika tamasha hilo.  Masanja na wenzake wakiwa wanasubiri zamu yao ya kuimba waliutumia wakati huo kununua mapambo hayo.

Hata hivyo, baadhi ya watu waliofurika kwenye uwanjani hapo walionekana kushangwazwa na kitendo cha walokole hao kununua vitu hivyo walivyoviita vya kishetani.
...manunuzi yakiendelea.
Masanja akiwa katika suti yake nadhifu uwanja wa Jamhuri.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages