EXTRA BONGO, TWANGA PEPETA KUPIMANA UBAVU MORO MEI MOSI - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

EXTRA BONGO, TWANGA PEPETA KUPIMANA UBAVU MORO MEI MOSI

Matangazo ya burudani itakayotolewa na bendi za Extra Bongo na African Stars.
NA DUNSTAN SHEKIDELE, MOROGORO
BENDI mbili zenye upinzani mkali jijini Dar es Salaam, Extra Bongo 'Wazee wa Kisigino' na African Stars 'Twanga Pepeta’ wataonyesha makali yao mjini Morogoro siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) ambayo kitaifa itafanyika mkoani humo.

Bendi hizo ambazo zimesheheni wanamuziki nguli zitafanya shoo siku moja katika kumbi tofauti ambapo Etra Bongo watakuwa ukumbi wa Savoy uliopo katikati  ya mji ambapo Twanga Pepeta watakuwa maeneo ya Nane Nane ukumbi wa Groness.

Bendi hizo zimekuwa “zikiibiana” wanamuziki kila mara kiasi cha kuzifanya ziimarike zaidi na hivyo kuzua ushabiki mkubwa wa wapenzi wa muziki nchini.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages