GLOBAL MISS DAR CITY CENTRE YAPAMBA MOTO - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

GLOBAL MISS DAR CITY CENTRE YAPAMBA MOTO

 
Mratibu wa shindano hilo Fatma Abdalah ‘Fetty’(mbele), akiwa kwenye pozi la pamoja na washiriki hao.
SHINDANO la kumasaka mrembo wa kitongoji cha Miss Dar City Centre 2011,  linazidi kupamba moto kutokana na purukushani za mazoezi yanayoendelea katika kambi yao iliyopo Lamada Hotel Ilala jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na mtandao huu jana, mratibu wa shindano hilo, Fatma Abdalah ‘Fetty’, alisema kwamba kila kukicha anazidi kuridhizishwa na uwezo wa  mazoezi ya warembo wake, na kwamba matumaini ya kutoa Miss Tanzania kwa kitongoji chake ni makubwa.

“Kiukweli ninazidi kuridhishwa na uwezo wa warembo wangu kila kukicha, na kufuatia uzuri walio nao natumaini mwaka huu naweza kutoa Miss Tanzania katika kitongoji change.”

Fetty, aliongeza kuwa hadi  kwenye  baadhi ya vitongoji alivyozungukia hajaona mrembo mwenye sifa za kuwazidi warembo wake.

“Kusema kweli tangu nimeanza kuzungukia kambi na mazoezi ya waandaaji wenzangu sijaona mrembo yeyote mwenye sifa za kuwazidi waembo wangu,” alisema Fetty.

Warembo wakijifua na mazoezi ndani ya ukumbi wa Lamada Hotel jana.

 
‘Rais wa Manzese’, Hamad Ally ‘Madee’ (katikati), akiwa kwenye pozi na baadhi ya washiriki wa shindano hilo.

Picha/Stori: Musa Mateja/GPL

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages