Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji Dkt. Mary Nagu,akimjulia hali Saida Rajab, mgonjwa aliyekatika mkono wa kushoto aliyelazwa Wodi ya Mwaisela katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, baada ya kupigwa na bomu wakati wa mshike mshike uliotokea wiki iliyopita, Gongolamboto.
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dkt. Willbod Slaa, akiwa na baadhi ya Wabunge wa chama hicho, katika Hospitali ya Amana kwenye moja ya wodi ya wagonjwa walioathirika na mabomu wakati walipofika kuwatembelea waathirika hao wa mabomu jana mchana
Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji Dkt. Mary Nagu, akimjunia hali George Daud, aliyelazwa katika wodi ya Sewahaji Muhimbili kutokana na kujeruhiwa na bomu.
Ilikuwa ni ziara ya siku nzima kwa ajili ya kuwajulia hali waathirika wa mabomu, katika Hospitali za Muhimbili, Amana na Temeke, huyu pia ni mmoja kati ya waathirika hao.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)