MWILI WA DOKTA REMMY ONGALLA WAAGWA LEO BIAFRA KINONDONI - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

MWILI WA DOKTA REMMY ONGALLA WAAGWA LEO BIAFRA KINONDONI

Mzee Makassy, Mjomba wa marehemu
Dk Remmy Ongala akiwa msibani
Mjane na watoto wa marehemu Dk Remmy Ongala
ambaye alijaaliwa watoto sita
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Emmanuel Nchimbi, akitoa rambirambi za Serikali wakati wa kuuaga mwili wa marehemu Dk Remmy Ongala aliyefariki majuzi na kuzikwa leo kwenye makaburi ya Sinza jijini Dar. Shughuli ya kutoa heshima za mwisho ilifanyika uwanja wa Biafra, Kinondoni
Dk. Emmanuel Nchimbi akiongoza umati wa waombolezaji kutoa heshima za mwisho kwa Dk. Remmy Ongala uwanja wa Biafra Kinondoni leo. Kulia ni mtoto mkubwa wa Dk. Remmy, Kalimangonga Ongala ambaye ni mwanasoka nyota.
Mbunge wa Ubungo, Mh. John Mnyika na Mbunge wa Kinondoni Mh. Iddi Azzan wakititoa heshima zao za mwisho kwa Dk. Remmy Ongala
Mshirika wa karibu wa siku nyingi wa Dk. Remmy Ongala, Cosmas Thobias Chidumule, akiwa na uchungu wakati wa heshima za mwisho kwa besti wake waliefanya kazi kwa miaka mingi kabla ya wote kuokoka na kuanza kumwimbia Mungu
Toni, Mjane wa Dk. Remmy Ongala, akiwa ameghubikwa na huzuni
Mzee Jangala na wadau wengine kibao walijitokeza kumuaga Dk. Remmy Ongala
Umati mkubwa ulikuja kumuaga Dk Remmy Ongala kiasi hata ikabidi polisi waitwe kuweka mambo sawa
Jeneza lenye mwili wa marehemu Dk Remmy ambaye jina lake kamili ni Ramazani Mtoro Mungamba Ongala
mdau wa Radio Kilimanjaro ya Sweden
naye yupo kurekodi tukio hili
Wake kwa waume, vijana kwa wazee
walijitokeza kwa Dk REmmy Ongala
Cosmas Thobias Chidumule akiongea
kwa niaba ya wanamuziki wote
Toka shoto ni wakongwe Mzee Makassy, Tchimanga Kalala Assosa (wa tatu waliosimama) akifuatiwa na King Kikii, Kanku Kelly na Abou Semhando
Mmoja wa viongozi wa kamati ya Mazishi
John Kitime akiandaa kitabu cha maombolezi
Familia ya Dk. Remmy Ongala

Malkia wa Mipasho Khadija Omar Kopa
na wadau wengine wakiwa na huzuni
Waombolezaji wakiwa katika majonzi
Umoja wa kwaya ukimlilia Dk Remmy
kwa wimbo maalumu waliomtungia.
Kwa Hisani Ya Michuzi Blog

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages